SEKRETARIETI ya Maadili ya Viongozi wa Umma imesema ipo tayari kuhakiki
mali za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, endapo watapokea
malalamiko kutoka kwa wanaomtilia shaka.
Hivi karibuni wakati akitangaza orodha ya watu wanaotuhumiwa kuuza,
kuagiza na kutumia dawa za kulevya, Makonda alijikuta akiingia katika
vita ya maneno na wabunge.
Msingi wa vita yenyewe ni hatua ya baadhi ya wabunge kupinga utaratibu
alioutumia Makonda kuwataja