Wednesday 11 May 2016

WELBECK NJE KWA MIEZI TISA KIJUE KISA HAPA

Facebook page yetu like hapa
https://www.youtube.com/watch?v=cQFl2V9IFUA
Mshambuliaji wa klabu ya Arsenal na Uingereza Danny Welbeck hatocheza kwa miezi tisa baada ya kufanyiwa upasuaji kutokana na jeraha la goti.
Welbeck mwenye umri wa miaka 25 alipata jeraha la mguu wake wa kulia wakati timu yake ilipopata sare ya 2-2 dhidi ya Manchester City siku ya jumapili na hatocheza mchuno wa Euro 2016.
Klabu yake imesema kuwa ukaguzi uliofanywa umebaini kwamba aliumia vibaya na kwamba sio jeraha la

WEST HAM WAMLAZA MACHESTER UNITED

Bonyeza hapa kulike page yetu ya FACEBOOK

West Ham
Klabu ya West Ham United iliaga uwanja wake wa nyumbani wa Upton Park kwa kuvuruga juhudi za Manchester United za kutaka kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Jumanne.
Ilikuwa mechi ya mwisho kuchezewa uwanja huo ambao umetumiwa na West Ham kwa miaka 112 kabla ya kuhamia uwanja wa Olimpiki.
Kwenye mechi hiyo ya kusisimua, West Ham walichomoza na ushindi wa 3-2.
Vurugu zilitokea kabla ya mechi.
Vijana wa Louis van Gaal walifahamu kwamba ushindi dhidi ya klabu hiyo na baadaye ushindi dhidi ya Bournemouth vingewahakikishia nafasi katika ligi kuu ya klabu Ulaya.

UJUE UKWELI JUU YA MWANAMKE ALIYEJIFUNGUA MAPACHA WATANO

FOLLOW US ON FACEBOOK BONYEZA HAPA
Bonyeza picha kuiona na kuskia maelezo kuhusu video mpya ya chura wa snura
https://www.youtube.com/watch?v=Zc8PxVw7c4gMama mmoja raia wa Australia ametoa picha za mapacha watano aliowazaa mwezi Januari.
Kim Tucci wa miaka 26 alichukua dadika mbili tu kujifungua wanawe hao, wasichana wanne na mvulana mmoja.
Wote walitungwa kawaida, hakutumia matibabu yeyote ya uzazi.

MWANAMKE WA MIAKA 70 KAJIFUNGUA HUKO INDIA

FACEBOOK
Unaweza pia bonyeza picha hii kujiunga na BZTV ONLINE ili usipitwe na matukio kwa njia ya video
Kaur
Mwanamke wa umri wa miaka 72 amejifungua mtoto mvulana katika hospitali moja nchini India.
Mwanamke huyo alipachikwa mimba kupitia njia ya kitaalamu ya IVF ambapo yai la mwanamke hutolewa kutoka kwenye ovari, kutungishwa mbegu ya kiume na kisha kurejeshwa kwenye mji wa mimba. Yai hilo linaweza kutolewa kwa mwanamke mwingine.
Njia hiyo hutumiwa kuwawezesha wanawake tasa kupata watoto.
Daljinder Kaur alijifungua mtoto wake baada ya kupokea matibabu kwa miaka miwili katika hospitali iliyoko jimbo la Haryana.

advertise here