Tuesday 6 December 2016

MATAIFA YA ULAYA KUTUMA CHOMBO SAYARI YA MARS

ExoMars
Mawaziri wa utafiti kutoka bara Ulaya wanaokutana mjini Lucerne, Uswizi wamesisitiza kwamba mpango wa kutuma chombo maalum kinachoweza kusafiri kwenye sayari ya Mars mwaka 2021 bado utaendelea.
Wameahidi kutoa jumla ya euro €436m ambazo zinahitajika kufanikisha mpango huo.
Mradi huo umechelewa kiasi na unagharimu pesa zaidi kuliko ilivyotarajiwa, jambo lililoibua wasiwasi kwamba mataifa wanachama wa Shirika la Anga za Juu la Ulaya (ESA) huenda wakaufuta

GARI LADUMBUKIA NDANI YA SHIMO HUKO TEXAS, MAREKANI

Mpita njia alisaidia mwenye gari jingine ambalo pia lilikuwa limetumbukia kwenye shimo hilo
Liwali ambaye hakuwa kazini alifariki baada ya gari lake kutumbukia kwenye shimo lililojaa maji, ambalo lilizuka ghafla katika eneo la San Antonio, jimbo la Texas nchini Marekani.
Maafisa wanasema Dora Linda Nishihara, 69, ambaye ni naibu liwali aliyekuwa anahudumu kama afisa wa kutekeleza maagizo ya mahakama, alifariki baada ya gari lake kutumbukia kwenye shimo

RIPORT YA HOSPITALI KUHUSU KIFO CHA MCHEZAJI WA MBAO FC KUFIA UWANJANI HII HAPA



Baada ya kufariki uwanjani kwa mshambuliaji wa timu ya Mbao FC Ismail Khalfan siku ya Jumapili ya December 4, leo December 6 2016 imetoka ripoti ya kilichosababisha kifo cha mchezaji huyo wakati wa mchezo kati ya Mbao FC dhidi ya Mwadui FC.

advertise here