
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni, na Michezo, Prof. Harrison Mwakyembe amesema kuwa anamshangaa Mbunge wa Jimbo la Chemba Mkoani Dodoma, Juma Nkamia kuhoji uwepo wake katika mkutano wa mwanamuziki wa bongofleva ‘Roma’ na waandishi wa habari uliofanyika juzi Jijini Dar es salaam.