Wednesday 12 April 2017

VIDEO: WAZIRI MWAKYEMBE AJIBU KWANINI ALIHUDHURIA ‘PRESS’ YA ROMA

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni, na Michezo, Prof. Harrison Mwakyembe amesema kuwa anamshangaa Mbunge wa Jimbo la Chemba Mkoani Dodoma, Juma Nkamia kuhoji uwepo wake katika mkutano wa mwanamuziki wa bongofleva ‘Roma’ na waandishi wa habari uliofanyika juzi Jijini Dar es salaam.

Video: MBUNGE WA NKASI ACHEKELEA ROMA KUPEWA KIBANO...ATAKA WASANII WANAOMTUKANA RAIS WAPEWE KIBANO ZAIDI


Mbunge wa Nkasi Kaskazini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ali Mohamed Keissy amefunguka na kusema wasanii ambao wanaandika nyimbo za kumtukana na kumkashfu Rais Magufuli wanapaswa kupata kibano zaidi ili waache tabia hiyo

Mbunge huyo amesema hayo leo bungeni na kusema angeaachiwa yeye dakika mbili tu wangeona ni nini angewafanya, hivyo kuendelea kuwatetea wasanii hao ni jambo ambalo si sawa, na kusema wasanii hao wajaribu kwenda Rwanda au nchi za kiarabu waone jinsi watakavyonyongwa.

ILE KESI YA GWAJIMA YA KUMTUKANA ASKOFU PENGO..LEO JAJI AMECHUKUA MAAMUZI HAYA MAZITO..!!!



Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeifuta   kesi ya kutoa lugha chafu inayomkabili Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima.

Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha aliifuta kesi hiyo leo chini ya kifungu cha 225 cha sheria ya Mwenendo wa Makosa ya  jinai (CPA).

Kesi hiyo imefutwa baada ya Wakili wa Serikali, Joseph Maugo kueleza kuwa hawakuwa na shaidi na kuomba wapewe ahirisho.

advertise here