Thursday 5 January 2017

JUNE 30 MWAKA HUU HIZI NDO SIMU ZITAKAZOIKOSA APP YA WHATSUPP


Kampuni ya Facebook inayomiliki huduma ya Whatsapp imesema kuna baaadhi ya simu za zamani zikiwemo zile zinazotumia mfumo wa Windows Phone 7.1, Android 2.2 na simu aina ya iPhone 3GS/iOS hazitakuwa na huduma za whatsapp kwa sababu wanataka kuendana na mifumo inayotumiwa na watu wengi.

ALICHOKISEMA YOUNG D KUHUSIANA NA TUHUMA ZA KURUDI KWENYE UNGA

Udaku,Young D

Hatimaye rapper Young Dee amejibu kwa ufupi kuhusiana na tetesi kuwa amerudi tena kwenye matumizi ya dawa za kulevya.

Akiandika maneno mafupi sana kwenye post yake mpya ya Instagram, Young Dee amedai kuwa ‘muda utaongea.’

“Time will Tell… Mi sina tatizo na mtu… Tuombeane kheri tu…

WAZIRI MKUU AONYA UJENZI HOLELA MANISPAA YA KIGAMBONI

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgXh1Y-RieZHLCCKJBe1GIYvY74CIIUexiHhSLfWd9tJkJMFRxWjj0M0bLHFRDY6Ay7ei8jnN85gP7yX799HmcoXAT9OyBbIGDx7Oiyjy4sGbGbmsWRkIGVooizXOfzPBxOXsWG87UE_xs/s1600/1.jpg
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ameutaka uongozi wa Manispaa ya Kigamboni kuhakikisha unasimamia ujenzi wa kisasa na kutenga maeneo maalumu ya wazi katika manispaa hiyo, ili kuepusha makosa ya ujenzi holela yaliyofanyika katika maeneo mengine jijini Dar es Salaam.

Pamoja na hayo, Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa amesema manispaa hiyo mpya kwa sasa inakabiliwa na tatizo la ukosefu wa majisafi na salama na wakazi wake wanatumia maji ya visima pekee ambayo si safi na salama.

SHERIA YA OBAMACARE TRUMP KUITUPILIA MBALI KWA KISHINDO

Rais Barack Obama amewahimiza wanachama wa chama cha Democratic kupigania sheria yake ya bima ya afya ambayo utawala wa Donald Trump umeahidi utaibatilisha upesi baada ya kuingia madarakani.
Kwenye mkutano wa faraghani wa saa mbili, Bw Obama aliwahimiza wabunge wa chama hicho kuitetea sheria hiyo, huku wanachama wa Republican nao wakichukua hatua kufuta sheria hiyo.

advertise here