Sunday 27 November 2016

LIVERPOOL YAPATA PIGO

 Philippe Coutinho amepata majeraha mabaya wakati wa kipindi cha kwanza kwenye mchezo wa Liverpool dhidi ya Sunderland.

Uwanja wa Anfield ulizizima kwa ukimya wakati fundi huyo wa kibrazil akiwa chini huku wakiwa na shauku ya kutaka kujua itachukua muda gani nyota wao kurejea tena kwenye pitch.

SALAMU ZA RAMBI RAMBI DK MAGUFULI KWA FIDEL CASTRO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli, amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Raul Castro kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Cuba Mhe. Fidel Castro kilichotokea tarehe 25 Novemba, 2016. Katika Salamu hizo Rais Magufuli amesema;

"Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Fidel Castro. Kwa niaba ya Serikali, Wananchi wa Tanzania na kwa niaba yangu mwenyewe natoa pole nyingi kwako, familia, Serikali ya Cuba na wananchi wa Cuba kwa kumpoteza mtu muhimu.

MAKAO MAKUU YA TANESCO KUBOMOLEWA WAKATI WOWOTE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli amesema kuwa Jengo la Makao Makuu ya TANESCO lililopo Ubungo litabomolewa wakati wowote kuanzia sasa ili kupisha ujenzi wa Ubungo Interchange yenye ghorofa 2 mpaka 3 hali itakayopunguza msongamano wa magari kwenye eneo hilo.

advertise here