Friday 13 May 2016

YANGA SASA NI WA KWENYE PIPA TU

FACEBOOK PAGE

KLABU ya Yanga imepanga kufanya mabadiliko ya kulitumia basi lao ambalo walipewa na wadhamini wao Kampuni ya Bia (TBL) ambapo litakuwa maalum kwa mashabiki wao badala ya kutumiwa na wachezaji wao.

Hayo yamesemwa na Ofisa Habari wa Yanga, Jerry Muro alipokuwa kwenye uzinduzi wa Tawi la Yanga Uswazi Mbeya eneo la Sokomatola juzi Jumatano wakati Yanga ilipokuwa jijini hapa kucheza na Mbeya City katika mechi ya Ligi Kuu Bara.

Muro amesema uamuzi huo wameufikiria kwa kuwa wamekuwa wakitumia zaidi usafiri wa ndege ambao umezaa jina la wao kuitwa wa kimataifa pamoja na kushiriki michuano ya nje.

advertise here