Monday 13 February 2017

AC MILAN WAPANGA MIPANGO KWA SANCHEZ, LUKAKU



Klabu ya AC Milan imeripotiwa kuwa katika harakati za kutaka kuwasajili washambuliaji wanaocheza katika ligi ya nchini England Romelu Lukaku wa Everton pamoja na Alexis Sanchez wa Arsenal.
Wawili hao wanatajwa kuwa kwenye mipango ya klabu hiyo ya mjini Milan, itakapofika mwishoni mwa msimu huu, na tayari imearifiwa fungu la pesa limetengwa kwa ajili ya uhamisho wao.

DKT. SLAA AMTUMIA UJUMBE GWAJIMA KUHUSU DAWA ZA KULEVYA



Vita ya kupambana na dawa za kulevya nchini iliyopamba moto zaidi na kuzua mijadala tangu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alipoanza kutaja majina ya watuhumiwa imemuibua Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dkt. Wilbroad Slaa.
Dkt. Slaa ameibuka baada ya kutajwa na kuhojiwa kwa Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ambaye alikuwa rafiki yake na ‘muwezeshaji’ wake kabla siasa za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 hazijawageuza kuwa mahasimu.

advertise here