Wednesday 2 March 2016

PICHA 10 ZA HALIMA MDEE AKITOKA MAHAKAMANI

LAYIII
Leo March 2 2016 wabunge wawili wa chadema, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara Pamoja na Diwani wa Kata ya Saranga, Ephrein Kinyafu. Wamefikishwa mahakamani kwa ajili ya kujibu mashitaka ya kumjeruhi katibu tawala Mkoa wa Dar es salaam wakati wa uchaguzi wa Meya wa jiji la Dar es Salaam ulipoahirishwa. Watuhumiwa wote

KIJUE KISA CHA WABUNGE WA UKAWA KUSAKWA KILA KONA

LAYIII


Wakati baadhi ya wabunge wa upinzani wakishikiliwa na polisi ama kutafutwa kutokana na chaguzi kile kinachoelezwa ni vurugu kwenye chaguzi za Meya na wenyeviti wa halmashauri zinazoendelea, wale waliotolewa Bungeni kwa nguvu Januari 27, wote wametakiwa kufika Dar es Salaam  wahojiwe.
Mpaka sasa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, anashikiliwa na polisi kwa kile kilichoelezwa ni vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam kuahirishwa Februari 27, mwaka huu.
Mbali na Mdee ambaye jana ilidaiwa kuwa polisi walifanya ukaguzi nyumbani kwake pamoja na ofisini kwake huku kile wanachokitafuta kikiwa hakijulikani, Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema) na wa Ubungo, Saed Kubenea, pia inadaiwa wanatafuwa kwa sababu ya vurugu hizo.

advertise here