Saturday, 11 February 2017

HIKI NDICHO ALICHOKIANDIKA GWAJIMA BAADA YA KUTOKA KITUO CHA POLISI



Askofu Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na Uzima ameachiwa na Polisi leo jioni baada ya mahojiano yaliyodumu toka Alhamisi mchana kwenye kituo

KAMISHNA MPYA DAWA ZA KULEVYA AFUNGUKA




Dar es Salaam. Rais John Magufuli amemteua Rogers Sianga kuwa kamishna mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA).

Baada ya kuteuliwa Sianga alizungumza na Mwananchi na kusema kwanza anamshukuru Mungu kwa uteuzi huo na akaahidi kushughulikia kwa karibu kesi za vinara wa ‘unga’.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais jana, Gerson Msigwa ilisema Sianga atasaidiwa na Mihayo Msikela atakayekuwa Kamishna wa Operesheni na Fredrick Kibuta atakayekuwa Kamishna wa Intelijensia.

Uteuzi huo umekuja siku chache baada ya Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya (Chadema) kumtaka

SPIKA WA BUNGE AKEMEA TABIA YA WABUNGE KUKAMATWA KIBABE BUNGENI


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai amekemea tabia ya ukamatwaji wa wabunge wanapokuwa kwenye vikao vya Bunge na kusema kuwa jambo hilo ni kinyume cha sheria na utaratibu.


Akihitimisha mkutano wa sita wa Bunge, Ndugai amesema kama kuna kiongozi yeyote wa serikali anamuhitaji mbunge, anapaswa kutoa taarifa kwake kwanza badala ya kwenda

Friday, 10 February 2017

MENGINE YAIBUKA SHIRIKA LA NDEGE TANZANIA


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameagiza Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), kujiridhisha na kiwango cha mapato linayokusanya kwa usafirishaji mizigo iwapo kiko sahihi.

Majaliwa amesema hayo alipotembelea makao makuu ya ATCL jijini Dar es Salaam kujionea utendaji tangu lilipoboreshwa mwaka jana kwa kununuliwa na Serikali ndege mpya mbili.

Waziri Mkuu amemtaka Kaimu Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa ATCL, Witness Mbaga kuhakikisha anatekeleza suala hilo.


Pia, ametakaka viongozi wa shirika hilo kuhakikisha wanazingatia ratiba za njia na muda wa safari ili wasipoteze wateja.

Vievile amesema ataagiza uchunguzi ufanywe na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) utakaolenga kujua ukusanyaji mapato katika kipindi hicho.

Waziri Mkuu akasema Serikali haitakuwa tayari kushuhudia shirika hilo linakufa tena na kuwataka viongozi wahakikishe linaendeshwa kwa faida kwa manufaa ya Taifa.

MAJIBU YA MAALIM SEIF BAADA YA PROF LIPUMBA KUMTAKA WAYAMALIZE



Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana, ilisema Maalim Seif alitoa kauli hiyo kwenye ziara ya siku nne kwenye wilaya saba za mikoa mitatu ya Unguja.

Maalim alisema ataendelea kufuata taratibu za kisheria ili kuhakikisha chama kinamaliza moja kwa moja mgogoro aliodai umepandikizwa na CCM kupitia kwa Lipumba.

VURUGU ZATAWALA BUNGENI WABUNGE WAKIMPINGA RAIS..MABOMU YARINDIMA


Bunge la Afrika kusini jana lilijawa na vurugu kuipinga hotuba ya Rais wa nchi hiyo Jacob Zuma.

Wakati akianza kuhutubia alikatizwa na kelele za Wabunge wa upinzani, waliokuwa wakimkosoa.

Miongoni mwa ukosoaji dhidi yake kuhusiana na matatizo ya kiuchumi na rushwa,

Thursday, 9 February 2017

KATUNI KALI LEO..CHEKA,FURAHI,ONGEZA MAARIFA




WEMA, ZARI KUONANA 'LIVE' KWENYE AROBAINI YA MTOTO NILLAN

Akizungumza live kutoka Clouds Fm, Diamond ametamka rasmi kuwa staa Wema Sepetu ni miongoni mwa wageni waalikwa kwenye sherehe hiyo, kwa upande wa Zari Hassan nae amesema hana shida na ujio wa Wema Sepetu Kwenye Arobaini ya Nillan ambaye waliwahi kuingia kwenye bifu kipindi cha nyuma.

ANITHA ATENGEWA DAU LA ILIONI KUMI ACHEZE UTUPU HUKO NOLLYWOOD

anita-2  MSANII kutoka kiwanda cha filamu Nollywood, Anitha Joseph ametengewa dau la Naira milioni 1.4 (milioni 10 za Kibongo) ili acheze filamu za utupu nchini Marekani.
Kwa mujibu wa Jarida la Vanguard, Anitha anayependa kupiga picha akiwa ‘ameyabusti’ matiti yake, alikuwa akichati na jamaa kutoka Marekani, Kane na kumng’ang’aniza kucheza filamu hizo za utupu zitakazokuwa zikimuingizia

ZIGO LAMPAGAWISHA BOB JUNIOR KINOUMA NOMA

Stori: Na Andrew Carlos IJUMAA | ShowBiz
Ama kweli kuna watu wamejaaliwa! Msanii wa muziki Bongo, Bob Junior hivi karibuni alijikuta akishindwa kurekodi video ya wimbo wake wa Chukuchuku baada ya kuchanganywa na dada mmoja aliyemtumia

TUNDU LISSU NAYE ATOKA POLISI KWA DHAMANA YA SHILINGI MILIONI 20

https://www.youtube.com/watch?v=GdoKspsDky0
Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka manne ya uchochezi.
Wakili wa Serikali Kishenyi Mutalemwa aliwasilisha maombi ya kupinga dhamana yaTundu Lissu kwa madai kwamba amekuwa na mwenendo unaohatarisha amani si tu

ASKOFU GWAJIMA AMFYATUKIA MAKONDA SAKATA LA KUTAJWA DAWA ZA KULEVYA

https://www.youtube.com/watch?v=GdoKspsDky0Gwajima:- Namuomba Rais ambadilishie Kazi Makonda, hii ya Ukuu wa Mkoa kutawala na kuongoza hata watu usiowapenda imemshinda. Sisemi amfukuze hapana nasema ambadilishie Kazi.

Gwajima : Makonda ana chuki na wivu na mimi

Gwajima : alikasirika hata niliposhuka na helkopta yangu siku ya mechi ya viongozi wa dini na wabunge dodoma.

Gwajima : nilichelewa kidogo nikaamua kupanda helkopta yangu mpaka uwanjani kabisa.

LECEISTER CITY YAZIDI KULINDA HESHIMA YAKE



Leiceister city na Derby County wakichuana

Klabu ya soka ya Leiceister city hatimaye imeweza kulinda heshima katika uwanja wake wa nyumbani wa king power kufuatia ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Derdy County katika michuano ya mwaka huu ya FA CUP ukiwa ni mchezo wa marudiano kusaka nafasi ya kutinga Raundi ya 5 ya michuano hiyo.

Hadi dakika 90 za mchezo zina maliziaka timu hizi tayari zilikuwa zimefungana bao 1-

JINSI MANJI ALIVYO WASILI KITUO CHA POLISI KATI CHA DAR ES SALAAM



Mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuph Manji amefika kituo cha Polisi cha Kati leo saa 4:54 asubuhi kwa ajili ya mahojiano baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kumtaka afike polisi.

Manji amefika leo badala ya kesho ambapo yeye na wengine 64 walitakiwa kufika kituoni hapo.

Manji ambaye pia ni Mwenyekitu wa Klabu ya Yanga jana alizungumza na waandishi

MZEE WA UPAKO NAYE ALIWAHI KUWA MHANGA WA TUHUMA ZA MADAWA YA KULEVYA

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) Ubungo-Kibangu jijini Dar, Lusekelo Anthony ‘Mzee wa Upako’ amejitaja kuwa ni mmoja kati ya watu mashuhuri ambao wamewahi kutuhumiwa kuhusika na biashara ya dawa za kulevya.
Amefunguka na kusema kuwa yeye ni mhanga wa suala hilo jambo ambalo lilimpa wakati mgumu sana katika maisha na kumfanya kunyanyapaliwa na jamii pamoja na watu wake wa karibu wakiwemo wachungaji wenzake.
Mchungaji Lusekelo amesema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachofanyika kupitia ukurasa wa facebook wa EATV kila Jumatano.

Wednesday, 8 February 2017

RAIS MAGUFULI AFANYA ZIARA YA GHAFLA KUTEMBELEA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE WA JULIUS NYERERE



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipofanya ziara ya kushtukiza katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa Terminal III kuona maendeleo ya ujenzi unaondelea Jumatano February 8, 2017

USHAIDI DHIDI YA KESI YA SCOPIONI MAPYA YAIBUKA DAKTARI AIBUA USHAIDI MZITO


Shahidi wa nne katika kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kujeruhi inayomkabili Salum Njwete, ameieleza Mahakama kuwa mtu aliyehusika kumtoa macho Said Mrisho alikuwa ni mzoefu wa vitendo hivyo  na siyo wa kawaida.

Shahidi huyo, Dk Christine Mataka (52) ambaye ni daktari  bingwa  wa macho kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), alitoa maelezo hayo katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala alipotoa ushahidi dhidi ya mshtakiwa Njwete (34) katika kesi iliyopata umaarufu wa ‘kesi ya Scorpion’ kutokana na maelezo kwamba aliyefanya uhalifu huo ni Scorpion.

KUTAJWA KWA MBOWE DHIDI YA MADAWA YA KULEVYA BUNGE LIMENUKA


Hatua ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kumtaja Kiongozi wa Upinzani bungeni, Freeman Mbowe kufika katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapo kesho kuhojiwa, imewachefua baadhi ya wabunge.

Wabunge waliohojiwa mjini Dodoma jana, walisema kinachoendelea ni siasa badala ya uhalisia.

Mbunge wa Kigoma Mjini, (ACT – Wazalendo), Zitto Kabwe alisema kinachoendelea ni siasa za kuchafuana na kwamba Makonda ajiandae kubeba msalaba wake katika jambo hilo.

VIDEO MAJIBU YA YUSUPH MANJI BAADA YA KUHUSISHWA NA MADAWA YA KULEVYA

Mfanyabiashara Yusufu Manji amesema kuwa atakwenda Kituo cha Polisi kesho kama Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alivyotaka.
https://youtu.be/4lddMaRaAD4
Manji amesema kuwa pamoja na kuwa Makonda ametaka wafike Ijumaa yeye atakwenda kesho huku akihoji kuwa inawezekanaje wakaitwa watu 65 kuhojiwa kama hakuna shughuli za kufanya kwa siku nzima.
“Mimi nina nafasi mbili kwenye jamii, Mimi ni mtoto wa baba yangu na nafasi yangu ya pili mimi ni mwenyekiti wa Yanga na nyote mnajua ninavyoheshimiwa. Huwezi kunitangaza kupitia radio

VIDEO: ASKOFU GWAJIMA AJIBU MAPIGO KWA PAUL MAKONDA

0
GWAJIMA
Saa chache baada ya kutakiwa kufika polisi na mkuu wa mkoa kwa kutoa taarifa juu ya madawa ya kulevya,Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima,Josephat Gwajima Amepost Ujumbe picha huu ambao wataalamu wa mambo wanadai kuwa ni kama jibu kwa Mhe Makonda.

advertise here