Monday 9 March 2015

NI ZAMU YA MBWA SASA KUGUNDUA TIBA YA KANSA ACHANA NA PANYA TENA KUTEGUA MABOMU

Dog PetWatafiti wamekuwa wakigundua baadhi ya viumbe kutumika sehemu mbalimbali, tumeona panya wanaotegua mabomu,
Watafiti wa magonjwa ya Cancer Uingereza wanasema kuwa mbwa ana kitu cha ziada muhimu kwenye afya ya binadamu.
Utafiti wa wataalamu hao unaonesha mbwa anaweza kugundua saratani ya Tezi ya shingo ya binadamu (Thyroid) kwa kunusa tu, ambapo katika majaribio waliyofanya imeonekana 88% ya watu waliogundulika na mbwa walionekana kuwa na saratani hiyo baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kitaalamu.
Mbwa aina ya frankie kutoka Ujerumani alifundishwa kunusa mikojo ya watu wenye ugonjwa huo na majibu kuonesha kuna asilimia kubwa mbwa huyo anaweza kugundua watu walioathirika na cancer hiyo.
Wanasayansi wanaona kwa hii njia mpya huenda ikayasaidia maeneo mbalimbali duniani ambayo hayana vifaa vya kupimia ugonjwa huo.

No comments:

Post a Comment

advertise here