BONYEZA HAPA KUIONA VIDEO USIACHE KULIKE COMMENT NA KUSUBSCRIBE NASI Mkali wa wimbo ‘Kidogo’, Diamond Platnumz amethibitisha ujio wa mtoto wa pili kutoka kwa mpenzi wake Zari.
Diamond
Muimbaji huyo amesema yeye na mpenzi wake Zari wanategemea mtoto wa kiume.
“Yah kweli mimi ni baba kijacho,” Diamond alikiambia kipindi cha Leo
Tena “Natarajia Mama Tiffa anipatie tena mtoto mwingine, atakuwa wa
kiume,”
BONYEZA PICHA SUBSCRIBE NASI YOUTUBE Meneja wa mwanamuziki wa kimataifa Diamond Platnumz, Hamis Tale Tale
maarufu kwa jina la ‘Babu Tale’ hivi sasa yupo mikononi mwa polisi
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.
Babu Tale amekamatwa leo na kufikishwa mahakamani hapo ili ajieleze ni
kwa nini asifungwe kwa kushindwa kutekeleza hukumu ya Mahakama
iliyomwamuru alipe fidia ya Sh250 milioni kwa makosa ya kuvunja sheria
ya Hakimiliki.
Kipindi cha ujauzito kwa mama ni kipindi muhimu sana ambacho kwa wakati
huu mama hatakiwi atumie kitu chochote cha kujitibu bila ushauri wa
daktari kwani kinaweza kudhuru mtoto lakini pia kipindi cha ujauzito ni
kipindi ambacho mama hatakiwi kunywa kileo chochote kile unachokifahamu.
Sio bia, sio spirit, wala mvinyo au wine. wanawake wengi wa siku hizi
hubeba mimba bila kufahamu kwamba wana mimba na huja kugundua baada ya
mwezi mmoja au miwili baada ya kumshindilia mtoto pombe za kutosha.tabia
hii ina madhara makubwa sana kwa mama na mtoto kama ifuatavyo...
Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB), inawaarifu wadaiwa wote ambao mpaka hivi sasa hawajaanza kulipa mikopo waliochukua kipindi wanasoma, na wenye majina yao kwenye orodha hii kwamba wamevunja mkataba kutokana na sheria ya bodi hiyo No. 9 ya 2004 (kama ilivyorekebishwa) sehemu ya 19 (1).
Na wanataarifiwa kwamba, kulingana na sheria hiyo ya bodi (HESLB) No. 9 ya 2004, Bodi imedhamiria kutenda yafuatayo:-
(i) Bodi itachukua hatua za kisheria kulingana na kipengele cha 19 (a) (1) cha sheria ya bodi.
Utafiti uliofanywa na wanasayansi wa Japan umethibitisha kwamba kukaa kwa mda mrefu na kutazama vipindi vya televisheni kwa masaa mengi kunahatarisha afya kwani huhusishwa na maradhi yanasababisha mzunguko wa damu mwilini kutokuwa sawa.
Watafiti hao wanasema, hali hiyo pia huenda ikasababisha damu kuganda na kutengeneza vidonge katika sehemu kama vile miguu, na iwapo mgando huo utasukumwa na nguvu za mzunguko wa damu na kuingia sehemu kama vile mapafu, husababisha vifo.
Utafiti huo ulihusiha watu zaidi ya 86,000 ambao hupendelea kutazama televisheni katika mida mbalimbali kwa siku.
Kisha afya zao zilifuatiliwa kwa zaidi ya miaka 19 tangu mwaka 1988 hadi 1990.
Vitunguu ni zao la pili ambalo hutumika karibu kila siku katika mlo wa familia za kitanzania. Afrika Mashariki, na Dunia Nzima.
Vitunguu vina chukua nafasi kubwa katika matumizi ya mboga hasa kwa
wakazi wa mijini. Vitunguu hutumika katika kutengeneza kachumbari,
kiungo cha mboga, nyama na
Mwigizaji
wa filamu nchini Tanzania Jackline Wolper aliyekuwa akimuunga mkono
Edward Lowassa katika uchaguzi Mkuu 2015, ametangaza kujiunga na CCM
rasmi jana.Wolper alikaribishwa na mwenyekiti aliyemaliza muda wake Dkt Jakaya Kikwete baada ya
Mwanamuziki mashuhuri kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Koffi
Olomide amekamatwa na kuzuiliwa na maafisa wa polisi katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta.
Olomide amekamatwa muda mfupi baada ya kumaliza mahojiano katika kituo kimoja cha runinga jijini Nairobi.
Mkuu wa polisi nchini Kenya Joseph Boinnet alikuwa ametoa taarifa na kuwaagiza polisi wachukue hatua.
Rapper Chidi Benz amefunguka kwa kusema kuwa hakuna msanii wa Hip Hop
ambaye amefikia mafanikio yake huku akidai Joh Makini na Nay wa Mitego
wametengenezwa ili waje kulishika game la muziki.
Akiongea na Uhuru FM Alhamisi hii, Chidi Benz amedai mpaka sasa hakuna
msanii ambaye ameweza kufanikiwa na kufikia mafanikio ambayo aliyafikia
katika kipindi cha nyuma.
Mnamo mwezi Machi, 2016, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
ilitoa notisi ya siku 60 ikiwataka wanufaika wa mikopo ya wanafunzi wa
elimu ya juu kujitokeza na kuanza kurejesha mikopo yao.
Aidha, taarifa hiyo pia iliwataka waajiri kuwasilisha taarifa za
waajiriwa wao na makato ya marejesho. Baada ya kipindi hicho
kumalizika, kipindi cha notisi hiyo kiliongezwa ambacho pia kimekwisha.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Democrasia na Maendeleo CHADEMA ambaye
pia ni waziri mkuu mstaafu Mh. Edward Lowassa amelitaka baraza la
vijana la CHADEMA Taifa kutokukubali kugawanywa katika misingi ya
kisiasa na badala yake wajikite katika kukiimarisha chama hicho katika
ngazi ya chini hasa vijijini.
Aliye kuwa mshindi wa shindano la big brother africa linalo fanyika nchini africa kusini kila mwaka idriss sultan amekuwa akijizolea umaarufu kila kukicha kutokana na vituko anavyo vionyesha huko
Wakati akizungumza na Maafisa wa Jeshi la polisi aliowapandisha vyeo vya
Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa
Polisi (SACP) Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli alisema kipindi
cha nyuma jeshi la polisi lilikuwa linaweka historia mbaya.
Kuna baadhi ya polisi waliowahi kuumizwa siku za nyuma kutokana na
kusimamia sheria. Kuna magari au mabasi ya wakubwa ndani ya polisi
ambayo ilikuwa ukiyakamata unapata msukosuko kikazi na kimaisha.
Rais akatolea mfano akisema kulikuwa na mabasi yanayoitwa Buffalo, Happy
Nation au Happy Tanzania ambayo ukiyagusa lazima utaondolewa kwenye
cheo ulichopo.
Rais akawaomba Makamishna kwenda kufanya kazi bila woga na wahakikishe
pia hawawabughudhi Maaskari walio chini yao wakati wanatimiza majukumu
yao ndani ya sheria na Kanuni za utumishi wao.
VIDEO MAGUFULI AKIZUNGUMZIA KUHUSU SUKARI KAMA ULIKOSA KUIONA
‘’Hata kama askari atakamata gari la IGP, RPC, Waziri au Rais, mwacheni
atimize majukumu yake ili wahusika wa hayo magari wakajieleze wenyewe
mbele ya sheria. Sheria ni msumeno’’. Rais alisema.
Rais aliendelea kusema, ‘’tunawanyima nguvu hawa Maaskari wa chini
wanapotimiza wajibu wao kwa mujibu wa sheria halafu tunawaambia liachie
hilo gari. Akishatoka pale yule aliyekuwa amekamatwa huanza kutamba
kweli kweli huku askari akiwa amevunjika moyo na nguvu katika kusimamia
sheria. Niwaombe sana, Vyeo vyetu tuweke pembeni na sheria tuziweke
pembeni’’.
Jeshi la Polisi limekwama kuwafikisha mahakamani viongozi wanne wa Taifa
wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), baada ya kukosea hati ya
mashtaka.
Wanaoshikiliwa ni Mwenyekiti wa Taifa, Patrobas Katambi, Katibu Mkuu,
Julius Mwita, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Joseph Kasambala na
Mwenyekiti wa Mkoa wa Mbeya, George Tito.
Akizungumza jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa
alisema makosa
Tangu daraja jipya la Kigamboni lianze kutumika rasmi tarehe 19/04/2016
limekusanya jumla ya shilingi bilioni 1.3 kutokana na tozo za vyombo vya
usafiri.
SUBSCRIBE KTK CHANNEL YETU HAPA
Hivi karibuni kumekuwa na mabishano kwenye mitandao ya kijamii kati
ya video queen wa ngoma ya Nuh Mziwanda na aliyekuwa na mpenzi wake
Shilole, Nuh Mziwanda amepiga stori na Clouds FM.
Mziwanda Akiwa na video queen wa kwenye video ya jike shupa
‘’Wale ni wanawake kwahiyo zile ni tofauti zao kwahiyo siwezi
kuingilia na siwezi kuongea chochote yule demu mie nilimlipa pesa yake
ya video akafanya kazi yangu kamaliza masuala yake yanayoendelea
kimpango wake, kwahiyo siwezi kuingilia na wala sitaki kufuatilia na
wala sitaki kujua kwasabbau nimeshamalizana
subscribe katika channel yetu hapa
Msanii Young D ambaye siku za karibuni ameweza kuachana na matumizi
ya dawa za kulevya amefunguka na kusema kwa sasa ameamua kumrudia Mungu
ili kujijenga na kuzidi kujiimarisha zaidi kiimani ili asiweze kurudi
gizani alikotoka.
Young D
Young D amesema hayo kupitia kipindi cha Planet bongo kinachorushwa
na East Africa Radio, Young D anadai kuwa alikuwa anapigana vita kati ya
nafsi na roho kwa yeye kushinda vita hiyo imempa nafasi kuweza kutumia
muda wake wa ziada kusoma sana biblia na vitabu vya dini ili
kujiimarisha kiimani ili asiweze