Friday, 17 February 2017

BARABARA YA KONGWA ARUSHA KUJENGGWA KWA KIWANGO CHA LAMI

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali itaanza kufanya upembuzi na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kutoka Arusha – Kiteto – Kongwa ili ijengwe kwa kiwango cha lami.

Alitoa kauli hiyo juzi wakati akizumgumza na mamia ya wakazi wa mji wa Orkesumet, wilayani Simanjiro akiwa katika siku ya pili ya ziara yake mkoani Manyara.

Alisema serikali imepanga kuiombea fedha za kazi ya ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa km 430 kwenye mkutano ujao wa bajeti na kwamba imepanga kutafuta wakandarasi wengi na kuwagawa kwa vipande ili barabara hiyo ijengwe kwa kipindi kifupi.

“Barabara yenu nimeiona. Imo kwenye Ilani ya CCM. Ujenzi wake utaanzia Arusha –Mbauda –

NAPE AWATAKA WAANDISHI WA HABARI KWENDA NA WAKATI...ZAMA ZIMEBADILIKA



SERIKALI imesema sekta ya habari inakabiliwa na changamoto katika uwasilishaji wa taarifa kwa umma kunakotokana na kasi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia hivyo kuwataka wadau kujitahidi kwenda na wakati hasa kwa upande wa redio ili wasipitwe na wakati.

VILOBA KWISHA HABARI YAKE TANZANIA




Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuanzia Machi Mosi, mwaka huu Serikali itapiga marufuku pombe kali maarufu kwa jina la ‘viroba’.

Ametoa kauli hiyo wakati akizumgumza na maelfu ya wakazi wa mji mdogo wa Mererani, wilayani Simanjiro akiwa katika siku ya pili ya ziara yake mkoani Manyara.

“Kuanzia tarehe 1 mwezi 3 ni marufuku kuzaliwa viroba , tutakae mkuta na viroba sisi na yeye, wanaotengeneza pombe watengeneze pombe waziweke katika ukubwa unaokubalika. Sasa hivi viroba

Thursday, 16 February 2017

SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA RIDHIWANI KIKWETE AFUNGUKIA YAFUATAYO


Image result for ridhiwani kikweteMbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete amefunguka kuhusu madai ya baadhi ya watu kuwa ana utajiri wa kutisha na kwamba anamiliki mali nyingi, jambo ambalo limekuwa likifanya watu hao watilie shaka njia aliyotumia kupata utajiri huo.

Kikwete  amesema kuwa anashangazwa na dhana hiyo potofu inayojengwa na watu bila kujua ukweli wa mambo, ambapo ameweka wazi kuwa yeye ni kijana mpiganaji na mwenye kupenda mafanikio,

VIDEO: MAAMUZI YA MAHAKAMA KUHUSIANA NA KESI YA MANJI

Leo kwenye Mahakama ya hakimu mkazi kisutu Dar es salaam alifikishwa Mfanyabiashara maarufu ambaye pia ni mwenyekiti wa Club ya Yanga, Yusuph Manji ambaye alikua akishikiliwa na jeshi la Polisi kwenye sakata la dawa za kulevya.

SIRRO: JIPU LA MANJI LATUMBUKA LIVE ADAI YAFUATAYO

Hatimaye imedhibitika kuwa Mwenyekiti wa Timu ya soka ya Yanga na Mfanyabiashara mkubwa nchini Tanzania Yusuph Manji anatumia madawa ya kulevya na leo atapandishwa kizimbani kwa tuhuma hizo akiwa pamoja na watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa kwa sakata kama hilo.
Katika Kipindi cha michezo katika redio moja nchini Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna,  Simon Sirro amethibitisha kuwa vipimo vya Mkemia Mkuu wa Serikali alivyofanyiwa Manji

Wednesday, 15 February 2017

AUDIO: UMEIPATA HII YA BARNABA KUMFUMANIA MKEWE ISKIE HAPA



Mke wa Barnaba Akiwa na Bwana Mwigine 
Jana February 15 2017 kupitia XXL ya clouds FM, Soudy Bwown ametuletea U Heard inayohusu mwimbaji staa wa Bongofleva Barnaba kudaiwa kuachana na mke wake.

MANENO YA KIKWETE KUHUSIANA NA SWALA LA MADAWA YA KULEVYA



Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete, amefunguka kuhusu sakata la dawa za kulevya na kuipongeza serikali hususani Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kwa kuanzisha vita hiyo na kutaka wahusika wachukuliwe hatua.

Kikwete amefunguka hayo leo katika kipindi cha East Africa Breakfast cha EA Radio, kinachoruka kila siku saa 11:00 alfajiri hadi saa 3:00 asubuhi.

DIVA AFUNGUKA KUHUSU KUTAMANI KUDATE NA ALIKIBA

Mtangazaji wa kipindi cha Ala za Roho cha Clouds FM, Diva The Bosslady amefunguka kwa kudai kuwa katika mastaa wa muziki Alikiba ndiye msanii ambaye anatamani kudate naye.
Diva ambaye kwa sasa anatoka kimapenzi na muimbaji Heri Muziki, alikuwa host wa show ya Valentine’s Day iliyofanyika Jumatano hii katika ukumbi wa Next Door na kuhudhuriwa na mastaa mbalimbali.
Akiongea na waandishi kabla ya kwenda kusherehesha show hiyo iliyoandaliwa na Irene Uwoya, Diva alidai Alikiba ndiye msanii ambaye anatamani kudate naye.

BREAKING NEWS: MASOGANGE NDANI KWA SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA

TAARIFA zilizotufikia, zinaeleza kwamba video queen maarufu Bongo, anayefahamika kutokana na shepu yake matata, Agness Gerald almaarufu Masogange, anashikiliwa na Jeshi la Polisi, Kituo Kikuu (Central) akituhumiwa kuhusika na biashara na matumizi ya madawa ya kulevya.
Masogange alikamatwa na polisi jana usiku na taarifa zinaeleza kwamba, mpaka muda huu bado anashikiliwa central. Mwanadada huyo anaingia kwenye orodha ya wasanii wengine na watu maarufu Bongo,

HAKIMU NA KARANI KIZIMBANI KWA RUSHWA

https://www.youtube.com/watch?v=at4JVl5SZ38
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru)  mkoani Mara imewapandisha kizimbani Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo mjini Musoma, Swalala Mathayo (40) na karani wa Mahakama hiyo, Charles Masatu (56) kwa tuhuma za kudai na kupokea rushwa.
Mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Musoma, Richard Maganga, Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Marshal Mseja, alidai  watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaiwa  kuomba na kupokea rushwa ya

Tuesday, 14 February 2017

MAAJABU: MIMBA MIEZI 13 AJIFUNGUA CHUA NA MDUDU MWENYE MANYOA MEUSI


Na Ibrahim Yassin, Kyela
MKAZI wa Kitongoji cha Njisi, Kijijiji cha Kilwa, wilayani Kyela, Tummanye Makula (35) , amekaa na ujauzito miezi 13 na kushindwa kujifungua.

Hata hivyo, baada ya maombezi, alijikuta akijifungua chura na baadaye mdudu wa ajabu akiwa na manyoya meusi.
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki baada ya dada huyo kumpigia simu Mchungaji wa Kanisa la Tample Of Prayer For All Nations Church, Nabii Charles Mkuvasa wa mjini Kyela  akihitaji kuombewa.
Alicuhukua hatua hiyo  baada ya kukaa na ujauzito kwa muda wote huo na kushindwa kujifungua, licha ya

AMUUA MFANYAKAZI WA SHAMBA AKIZANI NI MNYAMA NGIRI



Watu nchini Afrika Kusini wamegadhabishwa, kufuatia taarifa za mwanamme mmoja, ambaye analaumiwa kwa kumuua kwa kumpiga risasi mfanyakazi wa shamba, akidhani kuwa mtu huyo ni ngiri.

Stephen Hepburn alifikishwa mahakamani ili kujibu mashtaka ya mauaji.

Yeye na mwenzake wa kike walikuwa wakiwawinda ngiri kwenye shamba moja lililo mkoa wa Limpopo kaskazini siku ya Jumamosi, wakati Jan Railo ambaye alikuwa na umri wa miaka 23 aliuawa.

VIDEO: ALIKOLAZWA MANJI ULINZI NI WA KUFA MTU HUKO MUHIMBILI TAASISI YA MOYO


Hali ya ulinzi imeimarishwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) alikolazwa mfanyabiashara Yusuf Manji baada ya kuugua ghafla akiwa polisi alikokuwa akihojiwa.

Manji aliyekuwa akihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapa alipelekwa hospitalini hapo juzi jioni akiwa ndani ya gari la wagonjwa aina ya Toyota Land Cruiser lenye nembo ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) huku gari lake aina ya Range Rover likifuata kwa nyuma.

Askari wenye sare na wengine wakiwa na mavazi ya kiraia nje ya wodi aliyolazwa mwenyekiti huyo wa

Monday, 13 February 2017

AC MILAN WAPANGA MIPANGO KWA SANCHEZ, LUKAKU



Klabu ya AC Milan imeripotiwa kuwa katika harakati za kutaka kuwasajili washambuliaji wanaocheza katika ligi ya nchini England Romelu Lukaku wa Everton pamoja na Alexis Sanchez wa Arsenal.
Wawili hao wanatajwa kuwa kwenye mipango ya klabu hiyo ya mjini Milan, itakapofika mwishoni mwa msimu huu, na tayari imearifiwa fungu la pesa limetengwa kwa ajili ya uhamisho wao.

DKT. SLAA AMTUMIA UJUMBE GWAJIMA KUHUSU DAWA ZA KULEVYA



Vita ya kupambana na dawa za kulevya nchini iliyopamba moto zaidi na kuzua mijadala tangu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alipoanza kutaja majina ya watuhumiwa imemuibua Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dkt. Wilbroad Slaa.
Dkt. Slaa ameibuka baada ya kutajwa na kuhojiwa kwa Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ambaye alikuwa rafiki yake na ‘muwezeshaji’ wake kabla siasa za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 hazijawageuza kuwa mahasimu.

Sunday, 12 February 2017

NAPE APIGA ‘STOP’ ZUIO LA TCRA KUHUSU TV ZA MTANDAONI




Siku chache baada ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kudaiwa kuzuia uendeshaji wa runinga za mtandaoni (online TV), Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ametengua zuio hilo.
Nnape ameeleza kuwa ameamua kusimamisha zuio hilo kwakuwa halitakuwa na tija kwa wakati huu kwani kanuni zinazotoa muongozo wa namna ya kuendesha maudhui ya mtandaoni bado ziko kwenye

KWA NJIA HIZI PESA HAZITAKUKWEPA KAMWE

IDEA ya Biashara ni moja ya mambo yanayo waumiza watu wengi sana, Na mara nyingi wazo la biashara linahitaji utafiti wa kina ili kuja na wazo lenye tija kwako na kwa jamii nzima

WATUHUMIWA 16 WAKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA MKOANI KAGERA



Jeshi la polisi kwa kushirikiana na jeshi la wananchi Tanzania,Magereza na uhamiaji wilaya ya Karagwe mkoani Kagera linawashikilia watuhumiwa wa madawa ya kulevya 16 wakiwemo watendaji wa serikali za vijiji wanaojihusisha na biashara haramu katika mpaka wa Tanzania na nchi ya Rwanda kinyume cha sheria za nchi.

PAUL MAKONDA AFUNGUKA KUHUSU KUHOJIWA NA BUNGE



MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema hawezi kufika mbele ya Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kuhojiwa kwa kuwa hajapokea barua ya kuitwa.

Akizungumza  jana jijini Dar es Salaam, Makonda alisema hatoweza kwenda mbele ya kamati hiyo bila barua rasmi iliyomtaka kufanya hivyo.

Bunge lililokuwa likiendelea na vikao vyake Dodoma kabla ya kuahirishwa juzi, lilipitisha uamuzi wa kuwataka Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alaxander Mnyeti, kufika mbele ya kamati hiyo na kuhojiwa kutokana na kauli walizozitoa, zinazodaiwa kuudharau mhimili huo wa dola.

advertise here