Thursday 25 June 2015

KAFULILA KAIBUA UFISADI MPYA BUNGENI

LAYIII
2014 itaendelea kukumbukwa kwenye ulimwengu wa Siasa Tanzania baada ya ishu ya ufisadi wa ESCROW kubeba headlines nyingi kutoka Bungeni Dodoma, na Mbunge ambaye ni kama alihusika kuianika ishu hiyo ni Mbunge kutoka Kigoma, David Kafulila.

David Kafulila kaibua mengine ya ufisadi Bungeni? Sikiliza mwongozo wake na majibu ya Spika na Waziri.. (Audio)

IMG-20150625-WA00162014 itaendelea kukumbukwa kwenye ulimwengu wa Siasa Tanzania baada ya ishu ya ufisadi wa ESCROW kubeba headlines nyingi kutoka Bungeni Dodoma, na Mbunge ambaye ni kama alihusika kuianika ishu hiyo ni Mbunge kutoka Kigoma, David Kafulila.
Imesikika tena sauti yake live on air kutoka ndani ya Jengo la Bunge Dodoma na hii ishu nyingine >>> “Imejitokeza sakata la ufisadi kwenye uagizaji wa Mabehewa, Ripoti ya uchunguzi kuhusu jambo hili ipo inaonesha Kampuni ambayo ilipewa tenda ya mabehewa imeleta mabehewa ya kiwango cha chini na ililipwa fedha kabla ya kuleta mabehewa“>>> Mbunge David Kafulila.
IMG-20150625-WA0013Ripoti haijawahi kujadiliwa hapa Bungeni, huoni kwamba ni muhimu jambo hili liletwe hapa lijadiliwe kabla ya mwisho wa uhai wa Bunge hili na tufanyie maamuzi”>>> Mbunge David Kafulila.
Huwezi kuleta hoja kwa mwongozo, sekta inayohusika ina wajibu kujua hiki kitu kama ni kweli au sio kweli.. hatuwezi kujiingiza tu kujadili. Kamati inayohusika kama wewe ulipata na wenyewe watakuwa wamepata zaidi” >>> Spika Anne Makinda.
Kafulila asingeipata taarifa hii kama PPRA ambayo iko chini ya Wizara ya Fedha haijapeleka Ripoti hii kwenye Kamati… Ripoti hii imetolewa sio siri, tumeikabidhi Wizara ya Uchukuzi ichukue hatua kwa sababu inahusu zaidi manunuzi kwa sababu ni sekta ya Uchukuzi lilikuwa linasimamiwa na Wizara ya Uchukuzi.. sio jambo la kufichwa” >>> Waziri Saada Mkuya Salum.
Sauti yote utaisikiliza hapa

 



No comments:

Post a Comment

advertise here