
WAZIRI
Mkuu, Kassim Majaliwa ameutaka uongozi wa Manispaa ya Kigamboni
kuhakikisha unasimamia ujenzi wa kisasa na kutenga maeneo maalumu ya
wazi katika manispaa hiyo, ili kuepusha makosa ya ujenzi holela
yaliyofanyika katika maeneo mengine jijini Dar es Salaam.
Pamoja
na hayo, Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa amesema manispaa
hiyo mpya kwa sasa inakabiliwa na tatizo la ukosefu wa majisafi na
salama na wakazi wake wanatumia maji ya visima pekee ambayo si safi na
salama.