Friday 22 April 2016

HATUA 26 ZA KUANZISHA BIASHARA NDOGO NDOGO

LAYIII

Zifuatazo ni hatua 26 za kufuata katika kuanzisha biashara ndogondogo ambazo zitakuwezesha wewe kuanzisha biashara yeyote kwa uraisi zaidi.

Hatua ya kwanza ikiwa imebeba hatua zote kwani biashara inahitaji utayari (kuamua) zaidi ya vitu vingine kama mtaji nk

Hatua ya ya 1: Kuamua kuingia katika biashara

Kuamua kuingia katika biashara ni majumuisho ya utayari wa kisaikolojia, kiakili, kiuchumi na kukabiliana na hatari au vitisho vyote vitakavyojitokeza kwenye biashara
Maamuzi yako na hasa maamuzi magumu juu ya aidha kufanya hiyo biashara au la si ile hali ya kuamua kufanya biashara tu, bali pia ni ile hali ya kukubaliana na ups and downs za biashara husika na kuwa tayari kujitoa mhanga zaidi.

Hatua ya 2: Kuchanganua uwezo na udhaifu wako

Maeneo manne ni muhimu yapatiwe taarifa halisi na kuchukua hatua ili uweze kumudu kufanya biashara husika

Mazingira wezeshi Mazingira pingamizi
Mazingira ya Ndani UwezoUwezo wako katika kuendesha biashara mfano: utaalam, vitendea kazi, kiwanja nk. UdhaifuUdhaifu wako katika kuendesha biashara mfano: ukosefu wa utaalam, vitendea kazi, kiwanja nk.
Mazingira ya Nje FursaKuwepo kwa sera nzuri, katiba nzuri, hali ya hewa nzuri, mwitikio wa jamii nk VitishoKutokuwepo kwa sera nzuri, katiba nzuri, hali ya hewa nzuri, mwitikio mbaya wa jamii nk

Hatua ya 3: Kupata mafunzo

Baada ya kujua udhaifu wako, pata mafunzo
Mfano:-        Ya kupata ufundi au kubadili mitizamo
Kupata utaalam wa kiufundi katika biashara husika

Hatua ya 4: Kupeleleza mazingira utakayofanya biashara

Ni lazima upeleleze ili ujue fursa na hatari zilizopo katika biashara hiyo. mfano hatari (Risks, constraints) zaweza kuwa ni sheria na sera mbaya za nchi, sheria na sera kandamizi za kimataifa, barabara mbovu, hali ya hewa mbovu nk. Unatakiwa kusijua zote hizo ili aidha uweze kuzikwepa au kuzikabili.
Fursa nzuri zilizopo zaweza kuwa ni sheria na sera nzuri, miundo mbinu nzuri, nk

Hatua ya 5: Kuchagua biashara gani ufanye

i)    Kuzalisha bidhaa (Manufacturing)
ii)   Kuchuuza (Kuuza bidhaa)
iii)  Kutoa huduma (Service)

Kuzalisha bidhaa
Kuzalisha bidhaa ni kutumia rasilimali watu na malighafi ili kutengeneza bidhaa ya kuuza kwa mlaji au mchuuzi. Bidhaa ni kama vyakula, vyombo, nk

Kuuza bidhaa (Trading)
Kuchuuza bidhaa zilizotengenezwa na wengine ili kupata faida. Unaweza uza moja kwa moja kwa mlaji au ukauza kwa jumla (whole sale)

Kutoa huduma (Service)
Kutumia ujuzi wako au wa wengine katika kuwahudumia watu na shida zao kwa malipo. Mfano kufundisha, kutibu, kusafirisha, kutumbuiza nk

Hatua ya 6: Utafiti wa soko (Market Survey)

Washindani wako, uwezo na udhaifu wao
  • Ukubwa wa soko
  • Mgawanyo wa soko
  • Aina ya soko/masoko
  • Tabia za soko
  • NK

Hatua ya 7: Mfumo wa biashara

Fuatilia maelezo ya kila mfumo ukitilia maanani faida na hasara za kila mfumo. Unaweza pia kumtumia mshauri wa masuala ya biashara kukushauri kulingana na mazingira yako utakayofanyia biashara.
Hasa unatakiwa kujua zaidi mambo ya kisheria katika mfumo utakaoamua kuutumia kuendehsa baishara yako ili isije ikakuletea shida huko mbeleni, maamuzi ya mfumo upi uuchukue inategemea zaidi sheria za ndani ya nchi husika, pia inategemea ukubwa wa mtaji wako nk.

Mtu mmoja (sole proprietor)

Faida yake
Kuanzisha ni rahisi
Maamuzi hupitishwa kwa haraka kwa hiyo hakuna urasimu
Hasara yake
Biashara ikipata shida mmiliki anahusika na hasara kama vile ya ufilisi nk

 Ushirika (>watu wawili) (partnership)

Faida yake
Kuanzisha ni rahisi
Maamuzi hupitishwa kwa haraka kwa hiyo hakuna urasimu
Hasara yake
Biashara ikipata shida wamiliki wanahusika na hasara kama vile ya ufilisi nk
Mikataba inayoingiwa na mmoja wa washirika huwabana na wengine wasiohusika

Kampuni ya umma (public companies)(zaidi ya watu wawili bila ukomo)

Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Ukomo wa ufilisi upo kwenye kampuni husika na sio wenye hisa
Ni rahisi kuvutia mitaji mikubwa kupitia masoko ya hisa
Hasara yake
Haina usiri hivyo ni hatari kwani washindani wa biashara husika wanaweza kutumia taarifa hizo kujipanga
Muda na rasilimali muda kupotea kwa shughuli za kihasibu na kazi za makaratasi

Kampuni ya binafsi yenye ukomo wa hisa

(private companies limited by shares) (watu wawili hadi 50)
Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Ukomo wa ufilisi upo kwenye kampuni husika na sio wenye hisa
Kazi za makaratasi ni chache ukilinganisha na makampuni ya umma
Mlolongo wa taratibu za kisheria ni chache ukilinganisha na makampuni ya umma
Hasara yake
Gharama katika kuanzisha tofauti na biashara binafsi
Huruhusiwi kuuza hisa katika masoko ya hisa
Kampuni li lazima angalau iwe na wakurugenzi, katibu na mhasibu
Ni lazima ifanyiwe ukaguzi wa mahesabu kila mwaka

Kampuni ya binafsi yenye ukomo wa udhamini

(private companies limited by guarantees) (watu wawili hadi 50)
Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Ukomo wa ufilisi upo kwenye kampuni husika na sio wenye hisa
Kazi za makaratasi ni chache ukilinganisha na makampuni ya umma
Mlolongo wa taratibu za kisheria ni chache ukilinganisha na makampuni ya umma
Hasara yake
Gharama katika kuanzisha tofauti na biashara binafsi
Huruhusiwi kuuza hisa katika masoko ya hisa
Kampuni li lazima angalau iwe na wakurugenzi, katibu na mhasibu
Ni lazima ifanyiwe ukaguzi wa mahesabu kila mwaka

Jumuiya (association)

Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Inavutia wahisani
Ni ya watu wachache waliokubaliana
Hasara yake
Ukiritimba katika kupitisha maamuzi
Ugomvi wa mara kwa mara
Haina kinga kwa waazilishi

Vyama vya ushirika

Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Inavutia wahisani
Ni ya watu wachache waliokubaliana
Hasara yake
Ukiritimba katika kupitisha maamuzi
Ugomvi wa mara kwa mara
Haina kinga kwa waazilishi

Mashirika yasiyo ya kiserikali

Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Inavutia wahisani
Ni ya watu wachache waliokubaliana
Hasara yake
Ukiritimba katika kupitisha maamuzi
Ugomvi wa mara kwa mara
Haina kinga kwa waazilishi
Ukishachagua mfumo mzuri wa biashara yako, unatakiwa kuanza mchakato wa kuisajili katika mamlaka ya usajili wa makampuni inayoitwa BRELA ambayo ofisi zake zipo Jengo la shirika –Dar es salaam

Hatua ya 8: Kuchagua sehemu ya biashara

Kama ni sheli itabidi iwekwe kando ya barabara yenye magari mengi

Hatua ya 9: Kuchagua teknolojia

Ni muhimu kuangalia, kama biashara yako inategemea kwa ukubwa wake teknolojia usiende haraka hapa, tumia wataalamu wa technolojia husika ujua pro and cons zake kwani ukiharakisha hapa utaingia gharama isiyotakiwa na kuibebesha biashara yako mzigo wa manunuzi ambao hazikutakiwa, lakini pia technolojia husika inaweza kuchangia katika kupata faidi kubwa au hasra kubwa. uwe makini hapa.
Teknolojia itasaidia kujua
a)    Aina ya  watumishi
b)   Aina ya vitendea kazi mashine  /mitambo
Mfano kilimo cha maksai na kukamua kwa mashine
Teknolojia nzuri ni lazima iwe na sifa zifuatazo
a)    Ni rahisi kutumiwa
b)   Iwe rahisi kupata msaada kama mafundi nk
c)    Iwe inaendana na tamaduni husika
d)   Iwe ni rafiki wa watu na mazingira
e)    Iwe na gharama ndogo za uendeshaji
f)     Inaendelezeka

Hatua ya10: Kununua mashine na vifaa

Mashine na mitambo mingine itategemea sana uchaguzi wa teknolojia hapo juu 8(i)
Mashine zote na mitambo ni lazima kuzingatia yaliyotajwa hapo juu 8(ii)

Hatua ya 11: Usajili wa biashara

Hii hufanywa mara nyingi kwenye manispaa husika. Leseni kwa wafanya biashara ndogondogo ni bure (biashara ndogondogo ni ile ambayo mauzo yake hayazidi Shs 20 milioni kwa mwaka)

Hatua ya 12: Kuandika Mchanganuo wa Biashara (Business Plan)

  • Baada ya kufanya hayo yote sasa ni wakati mzuri wa kuandika  mchanganuo wa biashara yako
  • Mchanganuo wa biashara ni maelezo ya kina ambayo inaonyesha biashara yako ilikotoka, inakokwenda, hali ya masoko, sekta, kifedha na uongozi wa biahara yako. Ni taarifa muhimu ya kuwavutia wawekezaji na watoa mikopo kama mabenki
Mambo muhimu ya kujua katika kuandika Mchanganuo wa Biashara
1. Kasha la nje
2. Maelezo wa biashara yako
3. Historia na maelezo ya biashara yako
4. Maelezo ya bidhaa au huduma ya biashara yako
5. Mchanganuo wa masoko
  • Washiriki, uwezo an madhaifu yao
  • Ukubwa wa soko
  • Mgawanyo wa soko
  • Aina ya soko/masoko
6.  Mkakati wa utekelezaji
  • Uongozi na usimamizi wa kazi
  • Uchambuzi wa madhaifu, nguvu, fursa na hatari zinazokabili biashara yako
  • Mkakati wa Uzalishaji
  • Mkakati wa kuuza
7.  Mpango wa fedha
  • Uchambuzi wa mahitaji ya mtaji
  • Wapi utatoa mtaji
  • Matumizi ya mtaji
  • Makisio ya Mauzo
  • Uchambuzi wa kurudisha gharama (break even analysis)
  • Makisio ya faida au hasara
  • Makisio ya mzunguko wa fedha katika biashara yako (cashflow)
  • Makisio ya oanisho la mali na madeni ya biashara yako (balance sheet)
  • Ulinganifu wa sehemu mbalimbali za biashara (business ratios)
8.  Viambatanisho
  1. Lesseni
  2. Cheti cha ulipaji kodi
  3. TIN
  4. Cheti cha usajili
  5. Mikataba
  6. Risiti za manunuzi hasa mali za Biashara
  7. Taarifa zingine ambazo hazikupata nafasi ndani ya mchanganuo huu
  8. Taarifa zingine zinazoweza kuifanya biashara au kampuni kuaminika zaidi

Hatua ya 13: Kupanga juu ya pesa.

Kutafuta mikopo kwa kufuata utaratibu wa taasisi za fedha husika
Taasisi nyingi huhitaji yafuatayo
  1. Dhamana ya mkopo
  2. Uzoefu wa biashara husika
  3. Mchanganuo wa biashara
  4. Maombi ya mkopo

Hatua ya 14: Ufahamu wa kiufundi.

Hii ifanywe ili mwenye biashara apate ufahamu wa kiufundi juu ya biashara yake hasa kutoka kwa taasisi husika au mshauri wa biashara (consultant).

Hatua ya 15: Kujua vyanzo vya nishati:

Kama ni umeme hakikisha iko sawa na umeme utakidhi matakwa ya biashara.
Kama ni mafuta uhakikishe mafuta inapatikana na bei haitaadhiri bei ya bidhaa

Hatua ya 16: Kuweka vifaa: (Machines installation)

Wataalam husika wafanye hii kazi

Hatua ya 17: Kuajiri wafanyakazi.

Wafanyakazi wako wengi mtaani, lakini kumpata mtu atakayekidhi matakwa ya biashara yako kwa maana ya ubora na kufikia lengo la uzalishaji inahitaji usambazaji wa taarifa kwa upana zaidi na kwa maeneo maalum ambayo unategemea wafanyakazi watoke. Mfano vyuoni, makanisani nk
Unashauriwa pia kutumia marafiki na ndugu wa karibu ili upate mfanyakazi ambaye ni bora zaidi

Hatua ya 18: Kujua upatikanaji wa malighafi/biadha/huduma

Kama unazalisha malighafi bila ubishi ni kiungo muhimu kwa biashara yeyote inayohusisha kuzalisha bidhaa. Vivyo hivyo kama unachuuza, sehemu ya kupata bidhaa kwa bei ya jumla ni muhimu uzijue na kuziweka kwenye database yako. Na pia kama wewe ni mto huduma, unatakiwa kujua utapata wapi huduma zitakazokuwezesha wewe kuwahudumia wateja wako vizuri.  Vyanzo vya kupata malighafi/bidhaa/huduma ni muhimu ijulikane na iwe ya uhakika.

Hatua ya 19: Uzalishaji mali

  • Uzalishaji wa majaribio , Kuuza kwa majaribio kutoa huduma kwa majaribio muda – miezi 2-6, nk
  • Kuanza biashara rasmi
  • Kutunza siri ya unavyozalisha au kutoa huduma tofauti na wengine
  • Tunza vizuri siri zingine za biashara yako

Hatua ya 20: Kuhakikisha bidhaa yako hainakiliki

  • Kama unatengeneza biadhaa hakikisha fomula na mbinu ulizotumia ni ngumu na zimefanywa siri kubwa
  • Pia hakikisha unalinda hati miliki ya huduma au bidhaa husika katika ngazi husika za usajili na utambuzi

Hatua ya 21: Usalama wa biashara yako

Epuka majengo ambayo ni rahisi kuwaka moto, kubomolewa na wezi, wizi katika pesa za mauzo, utapeli wa bidhaa katika kununua na kuuza nk.

Hatua ya 22: Kuuza (Selling)

Kufikia wateja (fikiria utamfikiaje mteja wako wa kwanza – maelezo zaidi yatakuwepo katika mchanganuo wa biashara)
  • Kusambasa huduma/bidhaa
  • Kuweka bei
  • Kutangazia biashara
  • Promosheni nk.

Hatua ya 23: Utafiti wa soko (Market Research)

  • Hii ifanywe kila mara ili kujua kama wateja wamebadilika au bado Ili kujua kama wanapenda huduma/bidhaa zako au la.
  • Kujua biashara yako imekamata asilimia gani katika soko
  • Kupata maoni ya wateja ili kuboresha biashara/huduma/bidhaa
Namna ya kufanya utafiti

Utafiti wa kuendelea
Kila mteja anaponunua bidhaa, ajaze fomu maalum ya maoni. Mfano ya jinsi alivyohudumiwa, bei ya bidhaa, usindikaji, ubora nk
Utafiti maalum
Huu ufanywe wakati wa kutoa vivutiuo maalum au promosheni maalum.
Mteja wa promosheni ajaze fomu maalum ya maoni. Mfano ya jinsi alivyohudumiwa, bei ya bidhaa, usindikaji, ubora nk

Hatua ya 24: Kusimamia na kuthibiti biashara

Hii ni kuhakikisha kuwa biashara inakwenda kama ilivyobuniwa /pangwa. weka mifumo ya kudhibiti na kuhakikisha ubora unafikiwa nk

Hatua ya 25: Kutathmini biashara

Hii ni kujua kama biashara imekwenda kama ilivyobuniwa /pangwa.
Mambo ya kuangalia
  1. Mapato na matumizi
  2. Bajeti iliyopita
  3. Matokeo ya utaifit/wa soko

Hatua ya 26: Kufanya maboresho/mabadiliko

Unaweza kumuajiri au kumtumia mtaalam wa sekta hiyo kufanya taadhmini ya biashara yako.

Fanya sawa sawa na matokeo ya tathmini/utafiti

No comments:

Post a Comment

advertise here