Saturday 2 April 2016

GARI LA KIFAHARI LA POLICE LAMFANYA MKOSAJI ASAHAU FAINI HUKO DUBAI

LAYIII
Dubai ni moja ya sehemu ukienda kwa mara ya kwanza utajikuta unashangaa tu tena kama wewe ni mpenzi wa magari makali na maisha mengine ya kifahari ndio kabisa maana kuanzia watu binafsi mpaka Jeshi la Polisi wanayo magari ya kifahari kama Ferrari, Bugatti na Lamborghini ambayo wengi wetu tumezoea kuyaona kwenye video za mastaa wa dunia kama kina Nicki Minaj, Chris Brown na wengine.

Dubai ni moja ya sehemu chache duniani zenye usalama wa hali ya juu, mtaani hata iwe saa kumi au tisa usiku hakuna uhalifu na ninakumbuka mwaka 2014 nilifanya mahojiano na mwenyeji wa Dubai kwa zaidi ya miaka 20 akasema vitu kama wizi wa ukabaji au Majambazi hakuwahi kuvisikia, ishu alizowahi kuzisikia ni kama za visa vya mapenzi tu watu kupigana au kumletea mtu fujo sababu kakuchukulia mpenzi wako.
Kwenye hizi video hapa chini kuna Makala inayoonyesha Polisi wa Dubai wanavyofanya kazi na magari ya kifahari ya jeshi hilo ambayo yanaspidi kubwa kuliko magari ya kawaida lakini pia teknolojia waliyonayo kwenye kufatilia ishu za kiusalama.


No comments:

Post a Comment

advertise here