Tuesday 15 September 2015

JINSI AZAM FC NA MTIBWA SUGAR WALIVYOTIMIZA VIGEZO VYA KUPATA LESENI YA KLABU KWA 95% (+AUDIO)

LAYIII
Klabu za Ligi Kuu soka Tanzania bara bado hazijakidhi vigezo vya kupata leseni ya kudumu ya vilabu, kupitia kwa mkuu wa idara ya habari wa shirikisho hilo Baraka Kizuguto amethibitisha vilabu vingi kushindwa kupata leseni za vilabu isipokuwa klabu ya Azam FC na Mtibwa Sugar.

Vilabu 14 vinavyoshiriki Ligi Kuu Tanzania bara vimeshindwa kukidhi vigezo vya kupata leseni za kudumu na kupewa leseni za muda kwa kipindi cha miezi sita ili viweze kutimiza vigezo hivyo na kuweza kupata leseni hiyo, vilabu vinavyotajwa kutimiza vigezo kwa asilimia 95 ni Azam FC pamoja na Mtibwa Sugar ambavyo vinamiliki viwanja vyao.
“Vilabu vya Ligi Kuu kwa asilimia 95 hadi 97  hawajatimiza vigezo vya kupata leseni ya vilabu ukiondoa vilabu vya Azam FC na Mtibwa Sugar ambao wana  viwanja vyao hawa wamekidhi vigezo vya kupata leseni kwa asilimia 95, kilichofanyika ni kuwa kamati ya sheria na hadhi za wachezaji imetoa leseni ya muda wa miezi 6 kwa timu zote za Ligi Kuu ili kutimiza vigezo vya kupata leseni”>>> Baraka Kizuguto
Hii ni sauti ya Baraka Kizuguto


No comments:

Post a Comment

advertise here