Tuesday 18 August 2015

KAKOSA KAZI YA URUBANI NA KUISHIA JELA

LAYIII
baltic
Usafiri wa anga japo kumekuwa na Ripoti mfululizo kuhusu ajali za ndege lakini bado, usafiri wa anga unaendelea kuwa usafiri salama zaidi Duniani.

Sheria, kanuni na taratibu za usafiri wa anga zinafanya pia usafiri huo kuendelea kuwa salama zaidi, watu hawataki kabisa Rubani alete utani kwenye kazi !!
Rubani mmoja wa Kampuni ya Air Baltic pamoja na wenzake watatu walilewa pombe kama saa nne kabla ya kuanza safari na ndege ya abiria ambayo ilikuwa na abiria kama 100 hivi kutoka Norway, walipogundua kafanya kosa hilo walimzuia asiruke na ndege hiyo na ishu ikapelekwa Mahakamani.
Rubani huyo pamoja na wafanyakazi wenzake wengine wawili wamekiri Mahakamani kufanya kosa hilo, Mahakama imempa kifungo cha miezi sita jela alafu wenzake ambao ni wahudumu wa kwenye ndege hiyo mmoja amehukumiwa kifungo cha siku 45 mwingine siku 60.

No comments:

Post a Comment

advertise here