Monday 31 October 2016

KIPYA KUHUSU MISS TANZANIA 2016

Baada tu ya kutangazwa kuwa mshindi wa shindano la Miss Tanzania mwaka 2016, Mrembo Diana Lukumay alianza kupokea msg za taarifa zilizosambazwa mitandaoni kuonyesha kwamba alifeli kidato cha nne lakini pia pamoja na hayo bado CV yake ilionyesha anayo degree.
Diana ameamua kuweka kila kitu wazi kwa kusema ‘Jina langu ni Diana Loi Lukumay, mmasai na
umri wangu ni miaka 18, nilizaliwa Arusha Mount Meru Hospital na ni mtoto wa tatu kwenye familia ya watoto wanne’
3x6a0496
‘Nilisoma shule ya msingi ya serikali Levolosi 2005-2011, sekondari ya kutwa ya serikali Arusha 2012 -2015,  matokeo ya kidato cha nne nilipata darala la pili… nilichaguliwa kujiunga na kidato cha tano mchepuo wa Sanaa kwenda shule ya Wasichana Bwiru Mwanza’
‘Kwakuwa nilikua tayari nipo kwenye tasnia ya urembo niliamua kutojiunga na masomo hayo kwakuwa yalishaingiliana na ratiba za mashindano haya katika ngazi ya kitongoji ambapo nilijiunga na kambi ya Miss Ubungo 2016/2017) – Diana
3x6a0614
‘Baada ya kuahirisha masomo ya kidato cha tano niliomba kujiunga na masomo ya ngazi ya cheti kozi ya maswala ya kodi katika chuo cha usimamizi wa fedha ambapo mpaka masomo yanaanza mwanzoni mwa October 2016 tayari nilikua kwenye kambi ya Miss Tanzania, mafanikio ambayo niliyapata baada ya kuibuka mshindi na kutangazwa kuwa lete Raha Miss Kinondoni 2016/2017’
‘Juhudi zangu hazikuishia hapo, nilipotangazwa mshindi sikubweteka na taji hilo bali niliendelea na kazi zangu za kijamii katika jamii yangu ya kimasai’
JIAMINI KUWA HATA WEWE UNAWEZA FATILIA VIDEO HII LIKE COMMENT NA SHARE

No comments:

Post a Comment

advertise here