Mamaake aliyekuwa mwanamuziki wa mtindo wa Rap Tupac Shakur ,Afeni Shakur amefariki akiwa na umri wa miaka 69.
Kaunti ya California imethibitisha kifo chake kupitia ujumbe wa Twitter.Hakuna maelezo zaidi yaliotolewa.
Alice
Faye Williams,alibadilisha jina lake na kuitwa Shakur akiwa mtu mzima
alipokuwa mwanaharakati wa kisiasa na kujiunga na vuguvugu la Black
Panther.
Alikuwa na mimba ya Tupac mwaka 1971 alipokamatwa na
kufungwa jela pamoja na wanachama wengine wa vuguvugu hilo na kukabiliwa
na mashtaka ya njama ambayo baadaye yalitupiliwa mbali.
Shakur alikuwa kigezo kizuri cha muziki wa mwanawe na alisimamia muziko wake baada ya kifo chake.
Tupac Shakur alifariki mwaka 1996 akiwa na umri wa miaka 25,baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana katika gari moja.
Mauaji yake bado hayajapata ufafanuzi.
No comments:
Post a Comment