Monday 25 April 2016

HIII NDO TIA SAHIHI YA UGONJWA WA BAWASIRI

LAYIII

BAWASIRI AU KUOTA KINYAMA SEHEMU YA HAJA KUBWA (HEMORRHOIDS)
Ni ugonjwa unaotokana na kuathirika kwa mishipa ya damu ya ndani au nnje ya haja kubwa wakati mwingine mishipa hiyo inaweza kupasuka /kuteleza na kuvuja damu kwenye njia ya haja kubwa na kasababisha kinyama au uvimbe

Ugonjwa huu wa bawasiri kwa lugha ya kitaalamu tunauita hemorrhoids ilhali katika lugha ya kingereza unajulikana kama piles,


Tatizo hili huwaathiri zaidi watu wazima kuliko watoto na makadirio kuwa karibia 50%ya watu wote wako hatarini kupata tatizo hili katika umri wa miaka 30_50

AINA ZA BAWASIRI
{1}BAWASIRI YA NDANI
hii hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa na huwa haiambatani na maumivu na wengi huwa hawajitambui kuwa Wana tatizo hili

Aina hii hutokana na kuvimba na kuharibika kwa mshipa wa artery za ndani ya mfereji wa haja kubwa

Aina hii ya bawasiri imegawanyika katika madaraja manne


  1. DARAJA LA KWANZA ~Hii ni bawasiri ambayo haitoki mahali pake pa kawaida.
  2. DARAJA LA PILI ~hii hutokea wakati wa haja kubwa na kurudi yenyewe baada ya kujisaidia
  3. DARAJA LA TATU ~hii hutokea wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kurudisha ndani yeye mwenywe
  4. DARAJA LA NNE ~hii ni bawasiri inayotoka na huwa ngumu kurudi

[2}BAWASIRI YA NJE
Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na huambatana na maumivu makali na kuwashwa kwa ngozi katika eneo la tundu Hilo pia husababisha mishipa ya damu (vena) kupasuka na damu kuganda na kasababisha Aina ya bawasiri iitwayo THROMBOSED HEMORRHOIDS

CHANZO CHA TATIZO LA BAWASIRI
Ugonjwa huu wa bawasiri mpaka sasa chanzo chake hasa hakijapatikana ila Kuna vitu ambavyo huwa chanzo na hukuweka katika hatari ya kupata tatizo hili

  1. KUFANYA MAPENZI KINYUME NA MAUMBILE
  2. TATIZO SUGU LA KUHARISHA
  3. UJAUZITO
  4. UZITO MKUBWA
  5. MATUMIZI YA VYOO VYA KUKAA KWA MUDA MREFU
  6. KUPATA KINYESI KIGUMU KWA MUDA MREFU


DALILI ZA BAWASIRI

  • kupata muwasho mkali katika eneo la juu la haja kubwa
  • kujitokeza kwa kinyama eneo la haja kubwa
  • kutokewa na kiuvimbe katika tundu ya haja kubwa
  • kupata kinyesi chenye damu
  • kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia 


MATIBABU NA JINSI YA KUEPUKA UGONJWA WA BAWASIRI
matibabu ya bawasiri hutegemea na Aina ya bawasiri, mara nyingi wagonjwa wa bawasiri hupatiwa tiba ya kukatwa kinyama na kushauriwa kuendelea na tiba ya vyakula Lakini tiba huwa haina matokeo mazuri kwasababu baada ya Muda tatizo hujirudia kutokana na kwamba hawajatibu chanzo cha tatizo hivyo tiba nzuri ya bawasiri ni kutumia dawa itakayotibu chanzo cha tatizo huku ukiendelea na tiba ya chakula, MFANO MZURI WA DAWA NI ALO SNACA NA ANION hizo zinatibu na kuondoa tatizo moja kwa moja hivyo ni vizuri kutumia dawa hizo ili kumaliza tatizo pamoja na hayo ni vyema ukazingatia mambo yafuatayo ili KUEPUKANA na ugonjwa wa bawasiri


  • ZINGATIA KANUNI YA CHAKULA BORA KWA KUPENDELEA KULA MBOGAMBOGA ZA MAJANI, MATUNDA NA NAFAKA ZISIZOKOBOLEWA
  • KUNYWA MAJI MENGI ANGALAU GLASI SITA HADI 12 KWA SIKU
  • EPUKA KUTUMIA MUDA MREFU CHOONI


MADHARA YA BAWASIRI
Ugonjwa wa bawasiri una madhara makubwa iwapo hautapatiwa tiba ya uhakika haya ni baadhi ya madhara ya bawasiri

  • KUPATA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME
  • KUPATA TATIZO LA KUSHINDWA KUHIMILI KINYESI
  • HUPUNGUZA MORAL YA KUFANYA KAZI KUTOKANA NA MAUMIVU
  • HUATHIRI KISAIKOLOJIA
  • MWANAMKE HUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA

No comments:

Post a Comment

advertise here