Wednesday 2 September 2015

BILIONEA ROSTAM AZIZI AMUUMBUA DOKTA SLAA,ASEMA NI PADRI MUONGO WA KUPINDUKIA

layiii
Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi (kushoto), akisalimiana kwa kumbatiana na Mfanyabiashara maarufu nchini, Rostam Azizi 
ambaye pia ni mmoja wa wamiliki wa vyombo vya habari.picha na maktaba
NA KAROLI VINSENT
SIKU  moja kupita baada ya aliyewai pata kuwa Katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema Dokta Wilbroad Slaa kumtuhumu mfanyabishara maarufu Afrika, Bilionea Rostam Azizi akidai kuwa alimtishia maisha pamoja na kusema kuwa Mfanyabiashara huyo ndio anayeifadhili Chadema kwenye Kampeni zinazoendelea nchini.
        Hatimaye Bilionea huyo ameibuka na kusema Doka Slaa ni muongo na mpotoshaji na anayee faa kupuuzwa.
         Kwa mujibu ya taarifa ya Rostam Azizi Iliyotolewa kwenye vyombo vya Habari  nchini inasema kuwa  tuhuma anazotoa Dokta Slaa ni taarifa za uongo na zilizojaa chuki binafsi  na azipaswi kutolewa na  Mtu anayesema ni kiongozi wa kiroho ambaye ni Padri,
          Taarifa hiyo ya Azizi imesema kama Dokta Slaa anahushahidi kwa hayo anayomtuhumu  atoe ushahidi hadharani, kwani asihishie kutoa uongo mbele za watu akidai yeye Rostam hajawai kuifadhili chadema na wala hata kumtishia maisha mwanasiasa huyo aliyekimbia siasa.
         Amesema si kwa mara ya kwanza Dokta Slaa kumtuhumu mfanyabiashara huyo mashuhuri Afrika mashariki na kati kwa ujumla kwani amedai Slaa aliwai kumshutumu pia mwaka 2010 mara baada ya kumalizika uchaguzi mkuu akisema Rais Jakaya Kikwete,Edward lowassa pamoja na yeye Rostam Azizi kuwa walikutana kwenye hoteli moja jijini mwanza na kupanga mikakati ya kumwibia kura zake.
         Akidai siku hiyo anayosema Slaa hakuwepo nchini bali alikuwepo nje ya nchi.

      Taarifa hiyo imemazia kwa kuwataka Watanzania kumpuuza Dokta Slaa kwa kwakuwa ni miongoni mwanasiasa waliojaa uongo pamoja na upotoshaji  wakupindukia

No comments:

Post a Comment

advertise here