Tuesday 4 August 2015

KIJASHO KIDOGO CHAMTOKA PROFESA IBRAHIM LIPUMBA KISA KUMBEBA LOWASSA UKAWA

LAYIII

Taarifa za gazeti la Uhuru la leo ni kuwa Profesa Lipumba kajiuzulu uenyekiti CUF baada ya shinikizo kali kutoka kwa wanachama na viongozi wa CUF wasiotoa rushwa wala kupokea rushwa wa upande wa Zanzibar kutokana na sekeseke la yeye na al-maruhuni wenzie kumbeba Lowasa na kutaka awe mgombea UKAWA.
Kwa kujiuzulu kwake kunaonyesha wazi kuwa Lowasa kupitishwa na UKAWA itakuwa kazi ngumu kama CUF watatia ngumu UWEZEKANO AMBAO KWA SASA NI MKUBWA MNO.
Kama atakatwa basi safari yake ya Matumaini hewa sijui itaelekea wapi. Lakini taarifa zilizopo ni kuwa atatimkia ACT wazalendo kwa zitto kabwe kujaribu karata yake ya mwisho.




TETESI~Juma Duni Haji kuwa Mgombea Mwenza wa Lowassa
Mtakumbuka kuwa hapo awali kulikuwa na minong'ono kwamba Dr Slaa ndiye angekuwa Mgombea Urais wa UKAWA na mgombea mwenza wake angekuwa Juma Duni Haji. Hata hivyo, kutokana na Lowasa kuteuliwa kuwa mgombea Urais wa CHADEMA na ni dhahiri atakuwa mgombea wa UKAWA, Lowasa alimpendekeza Ismail Jussa Ladhu kuwa mgombea mwenza wake. Hata hivyo, taarifa zilizoripotiwa jana ni kwamba, Jusa alikataa pendekezo la kuwa Mgombea Mwenza na hivyo viongozi wa UKAWA wakampendekeza aliyekuwa Mwanasheria wa Zanzibar, Othman Masoud kuchukua nafasi hiyo.
Hata hivyo, taarifa mpya ni kwamba Othman Masoud naye amekataa pendekezo hilo kwa madai kuwa ana mambo mengi ya kitaifa na kimataifa yanamkabili. Kutokana na pendekezo hilo kugonga mwamba, ilibidi mpunga utembee. Jana muda wa mchana, Maalim Seif Sharif Hamad akitumia usafiri wa Makamu wa Kwanza wa Rais alienda Ofisi ya Lowasa iliyopo Masaki Dar es Salaam akiambatana na mwanasiasa mkongwe, Juma Duni Haji. Kwenye ofisi ya Lowasa alikuwepo Apson Mwang'onda, James Mbatia na Edward Lowasa.
Viongozi hao kwa pamoja walitumia muda mwingi kumshawishi Juma Duni Haji ili awe mgombea mwenza kama ilivyopangwa hapo awali. Hata hivyo, Juma Duni alionekana kukataa hasa pendekezo la kumtaka ahame CUF na kujiunga CHADEMA. Hata hivyo, viongozi hao walimhakikishia kuwa hakuna atakachopoteza na kwamba kwa vyovyote itakavyokuwa, uanachama wake wa CUF utalindwa. Lowasa alisema kuwa hawana muda zaidi wa kumtafuta mgombea mwenza na kwamba tumaini pekee limebaki kwake Juma Duni Haji.
Baada ya kutafakari kwa muda kidogo, Juma Duni Haji alikubali pendekezo hilo kwa masharti. Kwamba, apewe shilingi milioni 500 kama malipo yake kwa kukubali kujivua uanachama wa CUF. Pia endapo UKAWA hawatashinda nafasi ya Urais, awe analipwa mshahara wa shilingi milioni kumi kwa mwezi kwa kipindi cha miaka 5 ambacho atakuwa nje ya siasa za Zanzibar.
Masharti hayo yamekubaliwa na Lowasa ambapo jana Juma Duni Haji amepewa shilingi milioni 50 kama bonus na leo atapewa shilingi milioni 500 alizoomba na hivyo kufanya jumla ya kiasi chote atakachopewa kuwa shilingi milioni 550.
Kutokana na hali hiyo, Juma Duni Haji anatarajiwa kutangazwa rasmi leo Mlimani City Jijini Dar es Salaam ambapo CHADEMA wanafanya mkutano wa kumtangaza mgombea Urais na Mgombea Mwenza.
Kwa haya yanayoendelea, yanatukumbusha kitu kimoja cha msingi. Kwamba, CHADEMA hawakujiandaa kwa ajili ya kusimamisha Mgombea Urais na Mgombea Mwenza. Mgombea Urais katoka CCM na Mgombea Mwenza wamemwazima kutoka CUF. Hii inanikumbusha ya Mrisho Ngasa kuchezea Simba na Juma Kaseja kusajiliwa na Yanga.

No comments:

Post a Comment

advertise here