Sunday 9 August 2015

ILE COLLABLE ILIYOKUWA IKISUBILIWA KWA HAMU YA DIAMOND & ALI KIBA YATABILIWA KUVUNJA RECORD

LAYIII


 ALIKIBA Vs DIAMOND
Itakuwa ni bonge la hit song kama Diamond na Ali kiba watafanya Collable, na inawezekana wakapiga mpunga mwingi kupitia Collable hiyo, kwa sababu siku zote palipo na ushindani ndio pana maendeleo hilo halina ubishi, Muziki wa kizazi kipya hapa bongo umekuwa na ushindani wa hali ya juu kiasi kwamba hadi unatia faraja kwa wapenzi wa muziki huo, big up kwa wasanii wanao pigania level za kimataifa na kuipeperusha bendela ya Tanzania, kwasababu wanatoa changamoto kwa wasanii wengine ambao walikuwa wanafikilia kutoa nyimbo zenye mashairi ya kitoto na kuwafanya wabadilike na kutafuta tungo zinazo kubalika na jamii nzima
 Kwanzia mwaka 2014 mpaka kuingia 2015 Tz imekuwa ikitikiswa na wasanii wawili Diamond Platnumz & Ali Kiba katika anga za mabifu ya kimuziki ingawa  bifu lao ni lakitambo. Walikuwa ni marafiki wazuri tena wanapiga stori fresh na kupeana ushauri kama kawaida, ila walipo tibuana ndipo walipo anza kutengana na kila mmoja kuganga kivyake hadi sasa hivi wamekutana kwenye mlango  mmoja na kuanza kupambanishwa na mashabiki.
 Kwa sababu hiyo mashabiki wa muziki wa Bongo fleva hapa Tanzania walizidi kufurahia ugomvi huo wa kipekee ulio wafanya wasanii hao kila mmoja kukaa chini na kuandaa ngoma kali zaidi ili i-hit kuliko ya mwenzie, kingine ambacho kinawafurahisha mashabiki ni kuona ugomvi wao ni wakikazi na sio wa ngumi na matusi big up kwa Diamond & Ali kiba kwa ugomvi wenu wa kisomi.
 Hivyo basi tunajua kuwa Diamond na Ali kiba wote wanafanya muziki kwa ajili ya masilahi yao wenyewe na kilammoja anakubalika sana na mashabiki wake kutokana na kazi nzuri wanazo zifanya je?
  ukiwa kama mshabiki wa muziki huu utajisikiaje kama utazsikia breaking news kuwa Diamond & Ali Kiba wamefanya kolabo unadhani hiyo ngoma itachukua muda gani ku-hit? Toa maoni yako hapa.


No comments:

Post a Comment

advertise here