Monday 13 June 2016

NISHA KAMJIBU JACKLINE WOLPER WA HARMONIZE

SUBSCRIBE HAPA MTU WANGU
Staa wa sinema za vichekesho Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ ameibuka na kumjibu mwigizaji mwenzake, Jacqueline Wolper Massawe kuwa hajawahi kutaka ‘kiki’ za kijinga wala ugomvi na anachoangalia yeye ni biashara na maisha yanaenda.

Nisha aliliambia Wikienda kuwa ameshangazwa na habari zinazozagaa mitandaoni baada ya yeye kuweka picha za wasanii wanne kisha msanii mwenzake, Wolper kuanza kumrushia maneno wakati yeye aliandaa shoo ya Harmonize (mpenzi wa Wolper) wiki mbili zilizopita na yupo kibiashara zaidi
kwani bado ana shoo mbili ameandaa ikiwa ni pamoja na shoo ya mwezi huu wa Ramadhani ambayo itakuwa ni ya mahadhi ya mwezi huu.


“Huwa nawashangaa wasanii wengine, mimi sijawahi kupenda alipopenda msanii mwenzangu, tena ambapo ninajua kabisa kuwa huyu yupo huwa siingii kabisa kwa wakati huo, kama mnavyojua uhusiano wao uko wazi hivi naingiaje?

“Kuhusu kiki kuwa imepangwa ili kumuangusha Mr Blue na wimbo wake (Mboga Saba) ni ishu za uongo labda kama wamepanga wao,” alisema Nisha.

Chanzo cha maneno haya yote ni baada ya ujumbe unaosambaa mtandaoni kuwa Nisha alitaka kujiweka kwa Harmonize ndiyo maana akaandaa shoo kwao na msanii huyo ambapo Wolper aliishtukia na kuamua kuongozana na mpenzi wake huyo.
ULIPITWA NA SHOO HII HAPA CHECK HAPA MTU WANGU

No comments:

Post a Comment

advertise here