Thursday 5 May 2016

SNURA AWAOMBA RADHI WATANZANIA AKABIDIWA CHETI BASATA

SWAXBZ
13139342_1096943017015782_4396998989636500375_n[2]
Baada ya jana serikali kupitia Wizara ya Habari kutoa agizo la kumfungia Snura kutojihusisha na shughuli za muziki kutoka wimbo wake na kutojisajili Baraza la Sanaa Taifa (BASATA), leo mwanamuziki huyo na meneja wake HK wameomba radhi kwa umma katika Ukumbi wa Habari Maelezo, jijini Dar.

13165959_1096943100349107_1927214105826559228_n[2]
“Tumewaita Waandishi wa habari kwa ajili ya kuomba radhi kwa Umma na Watanzania kwa ujumla kwa kisa la kutengeneza, kuzindua na kuweka mtandaoni video ya udhalilishaji wa Mwanamke na isiyozingatia maadili ya Kitanzania ya muziki unaoitwa “Chura”.
13174026_1096943203682430_1720746537035521796_n[1]
Tunaviomba radhi vyombo vya Serikali vinavyosimamia sekta ya Sanaa kwa kutofuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo katika uendeshaji Sanaa nchini, mimi na meneja tunaahidi kutorudia tena kufanya tukio hilo la udhalilishaji, na iwapo tutarudia basi tupewe adhabu kali kwa mujibu wa sheria za nchi hii.” Snura
13139320_1096943067015777_1865714990596569862_n[1]

No comments:

Post a Comment

advertise here