Tuesday 2 February 2016

JE ILE VIDEO YA MBWANA SAMATTA ALIVYO TUA KULE KRC Genk ULIIKOSAA? ..... POA NIMEKUWEKEA HAPA

LAYIII
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania aliyekuwa anaichezea klabu ya TP Mazembe ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Mbwana Samatta January 29 taarifa za yeye kujiunga na klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji zilianza kuenea, na baadae kuthibitika baada ya picha za utambulisho wa staa huyo kuanza kuenea mitandaoni.
Huenda ilikupita au ulipata nafasi ya kutazama sehemu ndogo ya utambulisho wa Mbwana Samatta ambaye wengi tuliona akitambulishwa na kukabidhiwa jezi namba 77 tukiwa hatujui kwa nini kachagua jezi hiyo, Samatta ameeleza sababu ya kuchagua kuvaa jezi hiyo.
samatta
“Nimechagua jezi namba 77 kwa sababu wachezaji niliokuwa nawapenda mimi kama akina Eric Cantona, Cristiano Ronaldo na David Beckham walikuwa wanavaaa jezi namba 7, Mr Dimitri alivyoniuliza napenda kuvaa jezi namba ngapi nilimwambia jezi 77 kwa maana sikutaka kugombania namba ya jezi, kwa kila klabu unayokwenda ni ngumu kukuta jezi namba 7 haina mtu, sasa sikutaka kugombania namba ya jezi lakini mimi pia ni shabiki wa Man United” >>> Samatta
Video ya utambulisho na interview ya Samatta baada ya kutua KRC Genk


No comments:

Post a Comment

advertise here