Monday 5 October 2015

FAMILIA YA MAREHEMU MCHUNGAJI MTIKILA IMETOA MAJIBU KUHUSU KILICHOTOKEA KWENYE AJALI, KUAGA MWILI NA MAZISHI..

layiii
October 05 2015 ni siku ya pili inaisha tangu litokee tukio la ajali ya gari ndogo katika Kijiji cha Msolwa, Chalinze Mkoa wa Pwani ambapo ndani yake kulikuwa na watu watatu pamoja na Mwanasiasa Mkongwe Tanzania, Mchungaji Christopher Mtikila ambaye alifariki kutokana na ajali hiyo.
Tangu kutokea kwa ajali hiyo mambo mengi yameongelewa kuhusu ajali na kifo chake, mazingira ya ajali? Marehemu kutokuwa na jeraha? Mchungaji kufariki na wengine kupona? Ripoti ya Hospitali? Mazishi?
Familia ya Mchungaji Mtikila imeweka kila kitu sawa >>>> “Mchungaji Christopher Mtikila alipata ajali majira ya saa 11 Alfajiri eneo la Msolwa Chalinze, bahati mbaya alikuwa hajafunga mkanda na gari ilikuwa speed… Kulikuwa na gari llilikuwa lime-overtake upande wao, dereva wao akakwepa kwenda kushoto“.– Victor James Manyai, Msemaji wa Familia.
AW1A9946
Victor James Manyai, Msemaji wa Familia.
Hapa Msemaji wa Familia anasimulia mazingira ya ajali ilivyokuwa >>> “Eneo lile barabara imeinuliwa juu zaidi na eneo la pembeni limeshuka chini.. gari lilipaa juu, liliposhuka chini matairi yakapasuka yote, kwa sababu hakuwa amevaa mkanda akatokea mbele ya kioo cha gari.. alipoenda kuangukia, gari likaenda kumfunika upande wa kushoto, akawa hawezi kupumua“.- Victor Manyai.
unnamed (3)
Watu wengine walitoka na Majeraha kwenye gari, nini kilifanya Mchungaji afariki pekeyake? >>> “Ilichukua muda kwa sababu walikuwa watu wanne, mmoja alikuwa ameumia zaidi, mwingine alitupwa mbali… ilibidi mpaka wasamalia wema waje kusaidia kumuinua… walijaribu kumsaidia lakini hakuweza kupumua tena“.
AW1A9860
Baadhi ya waombolezaji wakiwa msibani.
Kuna stori kwenye Mitandao ya Kijamii kuhusu kifo chake huku wengine wakihoji kwa nini mwili wa Mchungaji Mtikila haujaonekana kuwa na majeraha yoyote? >>> “Mimi nilikuwepo katika Kikosi cha watu waliofanya postmortem pale Kibaha, tulikuwa na madaktari wanne, madaktari wawili wa Familia, mmoja wa Polisi na mmoja wa Hospitali ya Kibaha… sio kweli kwamba hana majeraha, alikuwa na majeraha kichwani na miguuni, ila siwezi kutaja siri za Marehemu ni kinyume cha maadili..Ukweli ni kwamba alikosa hewa, na kama kungekuwa na msaada wa dharura maisha yake yangeokolewa…“>>>
Mke wa Marehemu Mchungaji Mtikila.
Gari alilopata nalo ajali je? >>> “Ukweli ni kwamba gari lilikuwa limekodiwa, Mchungaji alikuwa na magari mawili na yote yalikuwa katika Kampeni Mkoa wa Mara na jingine Wilaya ya Kahama… Mimi ndio nilimkodia gari kwa madereva wa Taxi Mbezi mwisho, ni vijana ambao nawafahamu.” >>>
AW1A9886
Hii ndio Taarifa ya Familia kuhusu taratibu za kuaga Mwili wa marehemu na Mazishi >>> “Mwili wa Marehemu kwa sasa upo Hospitali ya Lugalo, Jumatano tutaaga mwili wa Marehemu Karimjee au Leaders Club, baada ya hapo tutasafirisha mwili kwenda Wilaya ya Ludewa, Mkoa wa Njombe” >>> Victor James Manyai, Msemaji wa Familia ya Marehemu Mchungaji Mtikila.
AW1A9858
AW1A9862
3X6A0398
3X6A0396
#RIP Mchungaji Christopher Reuben Mtikila.
Sauti ya Msemaji wa Familia imesikia kwenye Amplifaya October 05 2015, kama ulipitwa unaweza kuisikiliza pia hapa.


No comments:

Post a Comment

advertise here