Tuesday 8 September 2015

50 CENT KATIKA HEADLINE TENA ATANGAZA KUISHI KATIKA NYUMBA YAKE ILIYOPO AFRIKA

LAYIII
50 Cent siku zote ni mtu wa masuprise tu mtu wangu, mwezi July rapper huyo alitangaza kuwa amefilisika na idadi ya mali nyingi alizonazo si zake bali ni mali za mkopo, badaae tukasikia kuwa
anauza nyumba alioinunua kutoka kwa Mike Tyson mara tena tukasikia kuwa haiuzi tena bali anaitafutia mpangaji!
Headlines za 50 Cent zinazidi kuongezeka na mpya kutoka kwa 50 ni hii ya yeye kutangaza kuisha kwa nyumba yake mpya iliyopo AFRICA!
50Africa
Kupitia page yake ya Instagram @50cent aliandika… >>> “mjengo wangu uliopo AFRICA unakaribia kuisha, nitarusha party kubwa sana. Nitakuelezea badaae mtu wangu. Acha mzee nina maisha mazuri sana!”<<< @50cent.
50Africa2
Baada ya kuulizwa ukweli juu ya kufilisika kwake 50 Cent aliziambia blogs na websites nyingi kuwa; >>>“jamani sio kwamba sina hela, bali nimefanya hivi kulinda maslahi yangu ya kiuchumi pia kujipanga upya kibiashara, nimefanya hivi kujilinda”.<<< 50 Cent.
50Africa3
Hebu tazama hii video mtu wangu, alafu niambie unahisi hii nyumba inajengwa kwenye nchi ipi ya Africa.


No comments:

Post a Comment

advertise here