Friday 22 May 2015

SI WALIMU, WANAFUNZI WALA MADAKTARI SASA NI ZAMU YA WALEMAVU CHEKI KILICHOTOKEA JANA

LAYIII
Screen Shot 2015-05-21 at 3.19.05 PMWiki hii ilianza na headlines za migomo.. wa kwanza ulikuwa mgomo wa wanafunzi wa Chuo Kikuu Dar, ikafuatia
stori ya mgomo wa wanafunzi wengine wa Chuo Kikuu Saint Joseph.. ikasikika nyingine ya Polisi kuuzima mgomo uliotaka kuibuka Chuo cha Ruaha Iringa.
Kabla ya hapo mgomo mkubwa kabisa uliotikisa sehemu kubwa ya TZ ulikuwa mgomo wa madereva wa mabasi ya abiria ambao ulitokea mara mbili mfululizo.. leo hali haikuwa shwari Dar, kama ulitokea njia ya Buguruni kuelekea Kariakoo muda wa mchana palikuwa hapapitiki kabisa.
Screen Shot 2015-05-21 at 3.20.41 PM
Mgomo huu ulihusu wafanyabiashara wenye ulemavu ambao walikuwa na vibanda  vyao vya biashara eneo la soko la Karume, wanadai usiku wa kuamkia leo MAY 21 2015 Manispaa wamewavunjia vibanda vyao kinyume na makubaliano ambayo walifanya siku za nytuma kwamba watajadiliana kabla ya kuvunja.. wakaamua kufunga barabara eneo la Karume na kusababisha foleni kubwa ya magari.
Screen Shot 2015-05-21 at 3.18.25 PM
Baada ya zaidi ya saa nne kupita Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymond Mushi alikutana  na wafanyabiashara hao wakakubaliana kukutana kesho MAY 21 2015 ili kujadili jinsi itakavyofanyika ili walipwe fidia ya hasara waliyopata na kama kutakuwa na utaratibu mwingine wa kufanya ili kuwasaidia eneo la biashara zao.


Screen Shot 2015-05-21 at 3.19.05 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.18.51 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.19.05 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.19.20 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.19.34 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.19.50 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.20.03 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.20.29 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.20.54 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.21.39 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.21.51 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.22.09 PM
Screen Shot 2015-05-21 at 3.23.12 PM


Unahitaji chochote ninachokipata kisikupite? jiunge na mimi  

No comments:

Post a Comment

advertise here