Friday 28 April 2017

POLEPOLE AFUNGUKA HAYA MAPYA KUHUSU KATIBA MPYA YA WARIOBA..!!!




Akiwa ni miongoni mwa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amesema msimamo wake bado upo kwenye Rasimu ya Katiba hiyo.


Polepole aliipigia debe la nguvu rasimu hiyo ambayo miongoni mwa mapendekezo yake ni uwapo wa Serikali tatu; Shirikisho, Tanzania Bara na Zanzibar.

Akizungumza kwenye ofisi za gazeti hili wiki hii jijini Dar es Salaam, Polepole alisema msimamo wake bado uko kwenye Rasimu ya Jaji Warioba.

“Msimamo wangu ndivyo ulivyo muda wote tangu mwanzo hata sasa na CCM inaamini hivyo, kuheshimu maoni ya wananchi,” alisema Polepole na kuongeza:

“Hatuwezi kupuuza watu kwa namna yoyote, CCM haiko hapa kupuuza watu bali kuwasikiliza na ndiyo maana msingi wa mageuzi ya chama ni kuwa cha wanachama, unapokuwa na chama cha wanachama unakuwa daraja kati ya wananchi na Serikali.” 

Kuhusu utawala wa Rais John Magufuli kwa suala la Katiba, alisema kumekuwa na mageuzi yanayofanywa kabla ya kufikia kwenye mchakato wa Katiba.

Credit - Mwananchi


No comments:

Post a Comment

advertise here