Friday 6 January 2017

NICK MINAJ AELEZEA KUHUSU KUVUNJIKA KWA HUSUSIANO WAKE NA MEEK MILL





Baada ya kuwa na tetesi za kuachana kwa Hip Hop Couple ya Nicki Minaj na Meek Mill, Jan 5 2017, hatimae tumepata kauli ya mwisho kutoka kwa Nicki Minaj kuhusu tetesi hizo.
Mbali na kauli hiyo pia zilishaibuka tetesi Nov 21 mwaka Jana (2016) kuwa Nicki Minaj amempata mwanaume wa kumrithi Meek Mill baada ya kumpiga chini. Mwanaume huyo
aliyetwaja alikuwa ni Fetty Wap!
Fetty Wap & Nicki Minaj
Inshu hii ilitokana na vyanzo vilivyo karibu na Nicki Minaj ambavyo vilizungumza na mtandao wa udaku wa MediaTakeOut.com, ambapo ilidai kuwa Nicki ameanzisha uhusiano wa karibu na Wap, ambao vimedai ni mapema kuuita wa kimapenzi.
Rafiki wakaribu wa Nicki aliuambia mtandao huo, “They’re working on projects together, and maybe more, but we’re not ready to call them “dating” or “in a relationship” yet. Let’s see where [Fetty’s] head is at.”
Mzigo hukuishia hapo.. Chanzo kingine kilizungumza na mtandao wa HollywoodLife.com na kudai kuwa Nicki anapenda tetesi hizo ziendelee ili kumnyoosha Meek ambaye anadaiwa kumsaliti na mwanamke mwingine.
“She’s hoping it will light the fire under his a** so he realizes that she’s a queen and that he should do something about it,” kilidai chanzo hicho.
https://www.youtube.com/watch?v=9fu4Q0TuV5w
Meek Mill & Nicki Minaj
Sasa bad News ni kwamba, Kupitia kurasa yake ya Twitter Minaj amethibitisha kuwa ni SINGLE GIRL kwa kuandika maneno haya “To confirm, yes I am single. Focusing on my work & looking forward to sharing it with you guys really soon, Have a blessed New Year.”
Akimaanisha “Kuthibitisha, ni kweli niko single, juhudu zangu ni kwenye kazi sasa, hivi karibuni mtazisikia, muwe na mwaka uliobarikiwa“.
Nicki ’34’ na Meek Mill ’29’ wamekuwa kwenye mahusiano toka mwaka 2015. Mpaka sasa Meek hajasema lolote kuhusu kauli ya Nicki Minaj.

Alhamis hii, Meek aliweka picha Instagram ya viatu vyeupe brand ya Giuseppe Zanotti zenye mistari ya dhahabu na kuandika, “If you walk out don’t wear these, they wack.”
Viatu alivyoviponda Meek ni vile ambavyo Nicki Minaj alivivaa kwenye video ya wimbo wa mwaka 2013 alioshirikishwa na Ciara, I’m Out.
Wimbo huo una mashairi ya Minaj yanayosema, “You gon’ play me? / On Instagram, ni**as trying to shade me / But your bitch at home trying to play me.”
Nicki alidaiwa kummwaga Meek walipokuwa wakishereheka birthday ya mrembo huyo huko Turks and Caicos, wiki kadhaa zilizopita.

No comments:

Post a Comment

advertise here