Tuesday 24 May 2016

WAZIRI MKUU MSTAAFU AKIWA KATIKA KIBANDA CHA MPESA AKISUBIRI MUHAMALA WAKE




Waziri Mkuu mstaafu Mhe.Mizengo Pinda akiwa kibanda cha MPESA akisubiri kupokea malipo ya muamala wake. Hii ni mara ya kwanza kwa mtu aliyepata kuwa kiongozi mkubwa serikalini kuonekana hadharani akitumia huduma ya kutoa fedha kwa njia ya simu. Kwangu naona ni mfano bora kwa viongozi, kuishi REAL. 

Pia ni heshima kwa vyombo vya usalama kuweza kulinda usalama wa nchi na kuwezesha viongozi wastaafu kuingia mtaani na kufanya shughuli za kijamii bila kuhofia usalama wao. Pongezi kwa vyombo vya usalama. Si nchi zote zinaweza kufanya hivi. Haya ni maoni yangu. Nini maoni yako?? By Malisa G


No comments:

Post a Comment

advertise here