Wednesday 13 April 2016

MBONA HATUELEWI HAMA HAMA YA WATANGAZAJI A RADIO

LAYIII

Watangazaji sasa wanabadilisha vituo kama team za soccer.

Gadner katoka Efm kaenda Clouds.

PJ na Hando wametoka Clouds wameenda Efm.

Jabir saleh na Bi Hindu wametoka Times fm wameenda Efm.

Dj Senyorita na Mami wametoka East Africa radio wameenda Clouds.

Kuna tetesi Clouds sasa wanamtaka Kitenge kwa pesa yoyote anayotaka, Kitenge akichukuliwa na Clouds Shafii amesema ataondoka na Efm wanataka kumchukua kwa pesa ndefu.

Ni mwendo wa kutangaziana dau.

Hapa haieleweki ni jeuri ya pesa?

Stunt za kuongeza kusikilizwa?

Tasnia chovu ya utangazaji inakua?

Nani anaefaidika na hii game?

Au umjini mjini?

Efm wanakwambia huu mchezo hauitaji hasira!

Tusubirie kuona mwisho wa huu mchezo au labda ndio mwanzo wa sinema.

Mjini kuzuri sana!

Chanzo: Hapa

No comments:

Post a Comment

advertise here