Thursday 24 March 2016

ZITTO KABWE AFUNGUKA TENA KUHUSU RUSHWA KAMATI YA BUNGE AWATAJA TAKUKURU

LAYIII
BONYEZA PICHA KUJIUNGA NAMI YOUTUBE

Zitto juzi alitangaza kujiuzulu katika Kamati Bunge Huduma za Jamii aliyokuwa akihudumu kwa madai ya baadhi ya wajumbe kupokea rushwa.

Kupitia ukurasa wa mtandao wa kijamii wa 'Facebook' Mbunge Zitto amesema kwamba hatua inayochukuliwa na TAKUKURU ni hatua nzuri itakayopelekea ukweli kujulikana na watakaokutwa na makosa kuchukuliwa hatua stahiki.

''Uchunguzi wa vyombo vya dola ni moja ya njia muafaka ya kuhakikisha kila lisemwalo linakuwa na ukweli na pale ambapo suala limezushwa tu itajulikana na wazushaji hatimaye wataacha''-Amesema Zitto.
BONYEZA KUJIUNGA NA MERIDIAN BET UTENGENEZE MILIONI 10 KILA SIKU
https://meridianbet.co.tz/?affiliate=9051&campaign=8930&refer=aIQdLFigObtprhErnczA4A#!join
Aidha ikumbukwe kuwa baada ya tuhuma za rushwa katika kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii Mbunge Zitto Kabwe alimwandikia Spika wa Bunge Job Ndugai barua ya kujiuzulu akifuatiwa na Mbunge wa Nzega Mjini Hussen Bashe (CCM) ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo na ukweli uweze kufahamika.

No comments:

Post a Comment

advertise here