Wednesday 16 September 2015

TEKNOLOJIA INATUPELEKA HUKU SASAHIVI, SMARTPHONE INAJAA CHAJI KWA DAKIKA 35 MTU WANGU… (PICHAZ & VIDEO)

LAYIII
Watumiaji wa smartphones wakae tayari kuipokea hii good news mtu wangu, kuwa na smarthphone ni raha kwa sababu una uhakika wa kufanya mambo yako mengi sana kwa kupitia simu ya mkononi tu, ishu ni pale ambapo simu hizo zinamaliza chaji haraka na kujaa zinachukua muda pia
.
Phone IV
Huenda tukasaidiwa kwa upande mwingine mtu wangu, yani badala ya kusubiri simu yako kwenye chaji kwa saa mbili au zaidi ili ijae, tumetangaziwa kwamba mambo yatabadilika any time kuanzia sasahivi.
Phone V
Qualcomm Telecommunications Company ni kampuni ya Kimarekani ambayo inajihusisha na utengenezaji wa processor za simu, wamesema kwenye matoleo yanayofuatia wana mpango wa kutengeneza chip zitakazoweza kufanya smartphone ikaingiza chaji 80% kwa dakika 35 tu !!
Hiki hapa kipande cha Video, jamaa walivyoitangaza Teknolojia hiyo mpyampya mtu wangu !!


No comments:

Post a Comment

advertise here