Wednesday 16 September 2015

AJIKUTA MIKONONI MWA POLICE BAADA YA KUONYESHA UBUNIFU WAKE

LAYIII
Ahmed Mohamed ni kijana wa miaka 14, alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kufanya ubunifu ambao yeye alidhani itakuwa ni kitu kizuri kuwafurahisha Walimu wake, lakini baada ya kuwaonesha tu ubunifu wake, ikapigwa simu Kituo cha Polisi na wakamkamata !!

Ahmed ni mwanafunzi wa MacArthur High School iliyoko Irving, Texas Marekani… ni kijana ambae ana kipaji cha kufanya ubunifu wa kutengeneza vitu mbalimbali nyumbani kwao, alienda Shule na kisanduku kidogo ambacho alikifanyia ubunifu na kubadilisha kisanduku hicho kuwa saa.
Walimu walipomkuta na kifaa hicho walitoa taarifa Polisi, wakamkatamata ili akatolee maelezo vizuri kuhusu hiyo saa yake… kilichowashtua Walimu ni nyaya nyingi kwenye huo ubunifu wa saa, Polisi wanasema huenda huyo mtoto akafunguliwa mashtaka ya kutengeneza bomu feki na kuwatisha watu !!
Police Car
Ahmed amesema Polisi wamemhoji kwa nini ametengeneza Bomu? lakini amewasititizia mara zote kwamba kile kifaa sio Bomu ila ni saa ambayo aliibuni mwenyewe.
Polisi walimwachia huku uchunguzi ukiendelea lakini baba yake anaonekana kukasirishwa sana huku akihisi kwamba kuna ishu ya ubaguzi wa Kidini kwenye suala la mtoto wake kukamatwa kwa tuhuma hizo… Hii hapa Video ya Ahmed akijieleza ilivyokuwa.


No comments:

Post a Comment

advertise here