Sunday 13 September 2015

MATOKEO YA MAN UTD VS LIVERPOOL NIMEKUWEKEA HAPA

layiii
Ule mtanange uliokuwa unasubiriwa kwa hamu baina ya wapinzania wa jadi wa ligi kuu ya Uingereza, vilabu vya Manchester United dhidi ya Liverpool umepigwa usiku huu.

Mchezo huo uliopigwa katika dimba la Old Trafford umemalizika kwa Mashetani wekundu kuendeleza ubabe dhidi ya Liverpool kwa mara ya tatu mfululizo.
 
Daley Blind alianza kuifungia United goli la kwanza muda mfupi baada ya kipindi cha pili kuanza, kabla ya Ander Herrera kufunga la pili kupitia mkwaju wa penati.
Christian Benteke aliifungia Liverpool goli la kufutia machozi kwa mtindo wa ‘tik tak’ mwishoni mwa kipindi cha pili kabla ya mshambuliaji mpya wa Man United – Anthony Martial kufunga goli la 3 kwa United.
 

No comments:

Post a Comment

advertise here