Monday 3 August 2015

BREAKING NEWS!!! MAAMUZI MAGUMU YA CHADEMA DHIDI YA DR SLAA

LAYIII







Hatimaye baraza kuu la Chadema limeridhia kusimama kwa muda kufanya kazi za chama aliyekuwa katibu mkuu wa chama hicho Dr Wilbrod Slaa.
Ni kishindo cha baraka za baraza kuu la Chadema likiridhia kupumzika kwa Dk Wilibroad Slaa ambaye tangu kujiunga kwa wazir mkuu mstaafu Edward Lowassa amekuwa haonekani katika vikao vyetu vya chama hicho, katika ufunguzi wa mkutano wa baraza kuu la Chadema mwenyekiti wa chama hicho taifa Freeman Mbowe amekiri kuwa licha ya Dkt Slaa kushiriki vikao mbalimbali vya chama kuhusu ujio wa lowassa, lakini ni kweli alitofautian kimtizamo na wajumbe wa kamati kuu. 
 
Aidha Freeman Mbowe amekiri pia juu ya hofu iliyokwisha kutanda kwa viongozi, wanachama na wapenzi wa chama hicho juu ya ujio wa baadhi ya vigogo kutoka ndani ya chama cha mapinduzi CCM.
 
Kwa upande wake kaimu katibu mkuu wa Chadema taifa Salum Mwalimu akizungumza katika mkutano huo pamoja na masuala mengine amewataka wanachama na wapenzi wa chama hicho kuahkikisha wanaunganisha nguvu hasa katika kipindi cha uchaguzi.
 
Miongoni mwa agenda kuu zilizojadiliwa katika baraza kuu la Chadema ni pamoja na agenda ya kupitisha ilani ya chama hicho, kupendekeza majina ya wagombea nafasi ya urais ikiwa ni pamoja na kuthibitisha mikakati na rasilimali za kuendesha kampeni za uchaguzi mkuu. 

Tumekubaliana na Katibu Mkuu apumzike kwa muda, kwamba sis tuendelee na atakapokuwa tayari ataungana nasi mbele ya safari.Chama hiki hatukiendeshi kwa siri, tunakiendesha kwa mikakati.Mbowe-Tulilazimika kutumia kila mbinu halali ambayo inakiwezesha chama chetu kusaka matumaini na matarajio ya wananchi.Mbowe-Tuliridhika pasipo shaka kwamba ugeni wa Edward Lowassa katika chama chetu ni mpango wa Mungu.
Mbowe-Umoja wetu ndio ushindi, fursa iliyojitokeza ni nadra.
Mbowe-Mtikisiko huu umekuja kwa CCM kipindi ambacho Watanzania wanamatamanio ya mabadiliko 
Mbowe-Hatuwezi kuwa chama cha kuendelea kuhubiri mabaya ya jana tukashindwa kuhubiri maendeleo ya kesho
Mbowe- Kipigo wanachopata CCM, hawajawahi kukipata tangu tuanze siasa za vyama vingi
Mbowe-Kila tunayeweza kumpokea kutoka vyama vilivyo nje ya UKAWA tutamchukua
Mbowe-Mungu ameamua kutumia chama chetu kujeruhi na kuangusha CCM. 
Mbowe-CHADEMA ni chama cha siasa, ni chama makini, chama makinI ni chama cha watu, chama kisichokuwa makini ni chama cha viongozi.

Click image for larger version. 

Name: 11825867_894285133952134_6847320326544335608_n.jpg 
Views: 49117 
Size: 67.0 KB 
ID: 273255
   
Click image for larger version. 

Name: 11011569_894285180618796_3135540375877767017_n.jpg 
Views: 6937 
Size: 15.5 KB 
ID: 273256
   
Click image for larger version. 

Name: 11822332_894285227285458_674318579078359611_n.jpg 
Views: 28344 
Size: 71.6 KB 
ID: 273257
  
Click image for larger version. 

Name: 11822764_386120228247248_7723575338341037588_n.jpg 
Views: 4823 
Size: 64.7 KB 
ID: 273278
   
Click image for larger version. 

Name: 11825600_386111984914739_2411113025909127720_n.jpg 
Views: 4349 
Size: 72.6 KB 
ID: 273279
   
Click image for larger version. 

Name: 11825873_386111944914743_8869541588681525067_n.jpg 
Views: 4272 
Size: 82.8 KB 
ID: 273280
  
Click image for larger version. 

Name: 11828718_386111941581410_1907164532637209043_n.jpg 
Views: 4450 
Size: 79.3 KB 
ID: 273281

2 comments:

advertise here