Thursday 15 January 2015

MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI

HEKA HEKA MJINI NI HADITHI NZURI YA KUSISIMUA NA KU VUTIA
Nakumbuka vizuri ilikuwa siku ya jumapili ambayo kama ilivyoada kwangu huwa sikosi kwenda kanisani hasa misa ya kwanza kwani huwa napenda sana kusali misa ya kwanza ili baadaye niweze kuendelea na mambo yangu mengine,siku hiyo niliamka asubuhi na mapema kutoka pale nyumbani kwangu mnazi mmoja karibia na ofisi za chama cha mapinduzi za mkoa wa Dar-es-salaam na kuelekea kanisani pale saint.alban posta taratibu kwa miguu kwani gari yangu ilikuwa imeharibika wiki ya pili sasa na isitoshe pale nyumbani kwangu mpaka pale posta hapakuwa mbali sana kiasi cha kama dakika 20 tu hasa kwa kijana kama mimi ambaye damu ilikuwa bado inachemka.niliingia pale kanisani nikiwa sijachelewa sana misa ilikuwa imeanza kama dakika 7 hivi nakumbuka sana somo la siku hiyo alilolitoa padri Kiaka lilikuwa linahusu umuhimu wa kuombea siku yako ya kufa kwani haina siku wala saa.


Misa ilipoisha mida ya saa 3 asubuhi niliona nijivute mpaka mitaa ya upanga pale nyuma ya diamond jubilee mwendo wa pole pole nikamuone  rafiki yangu Martin ambaye pia alikuwa ni mfanyakazi mwenzangu. Sikutaka hata kumtaarifu kwenye simu kwani simu yangu haikuwa na pesa pia nilijua kwa kuwa tuliahidiana jana kwamba kesho nikitoka kanisani nitaenda kwake basi haina shaka nitamkuta tu kwani pia Martin huwa sio mzururaji sana hasa mida ya asubuhi kama haendi kazini.Wakati naingia ndani kwa rafiki yangu kipenzi  Martin nakumbuka ilikuwa ni mida ya saa 4 asubuhi mlangoni nilipishana na mdada wa makamo mweusi kiasi ambaye nakumbuka vizuri alikuwa amevalia dela la rangi ya kijani kibichi likiwa linamichirizi ya rangi ya zambarau na kwa ndani alikuwa amevaa suruali ya jeans ya rangi  nyeusi huku kichwani akiwa amejifunga mtandio mweusi kufunika nywele zake nilimsalimia aliitikia haraka haraka huku akikwepesha sura yake na huku akionyesha ni mtu aliyekuwa na shauku ya kuondoka lile eneo haraka sana, mimi hata sikumjali nilijua atakuwa ni mmoja kati ya wasichana ambao alikuwa na uhusiano nao bwana Martin kwa kuwa rafiki yangu Martin alikuwa ni mtu aliyependa sana wasichana,nilifika mpaka pale alipokuwa amepanga Martin ilikuwa ni nyumba ya uwani akiwa amepanga chumba na sebule huku nyumba ya mbele kukiwa hakuna mtu hata mmoja aliyekuwa amepanga kwa maelezo yake ile nyumba ya mbele kulikuwa na mpangaji lakini amehama na sasa mwenye nyumba alikuwa yupo akiifanyia marekebisho tayari kwa kuingia mpangaji mwingine. Ile nimefika tu mlangoni nikakuta mlango upo wazi kitu ambacho kikawaida sio busara kuingia nyumba ya mtu bila kugonga basi nikajivuta pale mlangoni na kuanza kuugonga ule mlango hallow Martin hallow  niligonga kama dakika tano bila kupata jibu lolote kutoka mule ndani ilinibidi nishangae kidogo kwa maana hata kama angekuwa msalani ni lazima angesikia ile sauti yangu na kwa nini akae kimya sikuamini kama alikuwa amelala wakati nimepishana na Yule dada anatoka chumbani kwake muda si mrefu,ikanibidi niingie tu ndani kama hayupo atanikuta mule mule nikimsubili, mungu wangu sikuamini nilipoingia pale sebuleni kwake nilikutana na michirizi ya damu kutoka pale sebuleni kuelekea chumbani kwake mh ikanibidi nipitilize haraka moja kwa moja kule chumbani kwake ile kuingia tu nikakutana na mwili wa Martin akinikodelea macho huku ukiwa umekakamaa huku pia ukiwa  umegandana na damu na alama kubwa ya kisu kwenye shingo yake,nilimkimbila pale alipokuwa amelazwa na kumuangalia mungu wangu alikuwa tayari ameshakufa,nilifikiria pale haraka haraka ni kipi nifanye nikaanza kuitafuta simu yake mule ndani mpaka nikaipata nikawapigia simu polisi na kuwaeleza lile tukio sikutaka nijihusishe moja kwa moja na lile tukio ndio maana niliamua kutumia simu yake pia simu yangu nilikuwa bado sijaweka vocha kisha nikaanza kutoka nje kabla sijatoka nje ya chumba chake macho yangu yakatua kwenye meza ndogo iliyokuwa mule chumbani kwake mara nikakutana na karatasi imeandikwa kwa Wino Mwekundu 
“NILIYEMUUWA NI MIMI MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI” shiti moyo ulijikuta unasisimuka na kuanza kudunda dunda kwani lile jina si mara ya kwanza kwangu kukutana nalo hasa kwenye kazi zangu,mungu wangu huyu mwanamke amemuuwa tena na Martin? Martini amemfanyaje tena huyu mwanamke hatari kama amemuuwa na Martin basi na mimi siku zangu haziko mbali hapana inabidi nimzibiti kwa kila hali nilijikuta nimekaa naangalia ile karatasi aliyoandika huku nikiutazama na mwili wake pale chini kwa muda wa dakika kadhaa mpaka machozi yakaanza kunitiririka kwa mbali,nilishitushwa na kelele zilizotoka nje nikahisi polisi watakuwa tayari wameshafika pale basi nikaona haina haja ya kuondoka tena nikachukuwa  shuka pale na kuanza kuufunika ule mwili hallow inspector vipi tayari umeshafika? Habari umeipataje? Ilikuwa ni sauti ya bwana Gerald mmoja wa ma afisa upelelezi pale makao makuu, ndio mimi niliyewapigia simu nilimjibu kwa mkato huku nikimsaidia kutoa vifaa vya kuchukulia finger print pamoja na camera digital ya kipelelezi kupiga picha mule chumbani kwa ajili ya kupata nyayo zake na alama zingine za Yule muuwaji,mkuu wangu wa kazi pia inspector Thomas na yeye pia alikuwa ni mmoja ya watu waliokuwa wamefika pale kwa ajili ya kushuhudia lile tukio wakati kina inspector Gerald wakiendelea kukusanya baadhi ya kumbukumbu mule ndani bosi wangu aliniita nje alipiga simu hospitali ya taifa ya muhimbili kuwajulisha kuhusu lile tukio kisha akaanza kuniuliza maswali kadhaa kuhusu lile tukio aliniuliza kwanza nilijuaje kama Martin amekutwa na lile tukio nikamjibu mimi mwenyewe imetokea tu kama bahati kwani tulikuwa tumepanga kukutana naye siku ya leo nikitoka kanisani ili tuelekee bagamoyo kusherekea siku ya mchumba wake ya kuzaliwa,ndio na mbona hili tukio tumejulishwa kupitia simu yake aliendelea kunihoji, ni mimi ndiyo nilitumia simu yake kuwajulisha kwani simu yangu haina pesa kabisa, je huyo muuwaji unamjua au unaweza kuwa unamhisi nani? Ni MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI bosi wangu alijikuta anashituka ohh wewe umejuaje? Aliniuliza kwa shauku kubwa ya kutaka kujua nimefahamu vipi aliyefanya lile tukio ni mwanamke mwenye kovu jeusi nikamwambia kuwa kama kawaida yake ameacha note juu ya meza mule chumbani mwa Martin ameandika kwa wino mwekundu, basi bosi wangu alinituma nikamletee ile karatasi aliyoiacha huyo mwanamke mwenye kovu jeusi,basi nilienda na kutoka nayo pale nje na kumpa aiangalie, aliiangalia kwa muda wa kama dakika 2 hivi halafu akaludisha macho kwangu na mimi muda ule nilikuwa pia nimemetolea macho basi tukajikuta tumetoleana wote macho,hivi hakuna anayemjua huyu muuwaji? Kwa maana sasahivi amezidisha haya mauaji alianzisha tena mazungumzo,

simjui ila uwezo wa kumpata upo kwa nini asipatikane kwa maana tukimchekea tutajikuta na sisi wote anatuondoa wakati nazunguma haya tayari gari ya kubebea wagonjwa kutoka muhimbili hospitali ilikuwa tayari imeshafika pale nyumbani kwa marehemu Martin tayari kwa kuchukua ule mwili kuupeleka hospitali ili ufanyiwe pia uchunguzi mwingine wa kitabibu .Wale manesi walishuka kutoka ndani ya ya ile gari ya kubebea wagonjwa na kuingia mule ndani tayari kwa kuuchukuwa ule mwili kwa ajili ya kuupeleka hospitali.
                             *************************************
NINI KITAENDELEA FUATILIA KISA HIKI KWA UMAKINI

No comments:

Post a Comment

advertise here