Sunday 13 November 2016

GIGY, AMBER LULU WAINGIA KWENYE VITA BARIDI

gigy_money
Gift Stanford ‘Gigy Money’.
Ma-video queen wasumbufu Bongo, Lulu Euggen ‘Amber Lulu’ na Gift Stanford ‘Gigy Money’ wapo kwenye vita baridi (vita ya maneno) kufuatia Gigy kumchamba mwenzake kutokana na yale
madai ya kukamatwa na ‘unga’ jijini Arusha.
amberlulu
Lulu Euggen ‘Amber Lulu’.
Chanzo makini kililiambia gazeti hili kuwa baada ya habari kuzagaa kuwa Amber Lulu amekamatwa na polisi Arusha akiwa na unga, Gigy amekuwa akimsema mwenzake huyo vibaya, mazingira yaliyosababisha wawili hao waanze kuraruana kwa maneno.
Akizungumza hivi karibuni, Amber Lulu alisema: “Nawashangaa hao wanaonisema vibaya kufuatia hizo tetesi, hasa Gigy ila siwezi kujibishana naye kwani siyo levo yangu.”
Gigy naye akafunguka: “Ni kweli nilimsema kuwa kama kweli kakamatwa na unga atakuwa katuaibisha sana. Huo ndiyo ukweli sasa akitokwa na povu atokwe tu.”
HUKUONA JINSI VISINGELI VINAVYO IMEZA DAR CHEKI HAPA

No comments:

Post a Comment

advertise here