Thursday 12 May 2016

YANGA ... NDANDA RUSHWA YAHUSKIKA............. ILICHOKISEMA SIMBA HIKI HAPA

FACEBOOK
unaweza bonyeza hii picha kujiuga nasi youtube
https://www.youtube.com/watch?v=V5T2IW-f2qg
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Jerry Muro amesema, Ndanda FC itakapoutumia Uwanja wa Taifa itamaanisha kwamba Ndanda FC watakuwa nyumbani na hata mapato katika mgao asilimia kubwa ataipata Ndanda hivyo haoni sababu ya wengine kuanza kuongea kwa kuona ni makosa katika mchezo huo.



Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Klabu ya Simba Zacharia Hans Pope amesema, mchezo huo ni sio halali kwani inaonekana ni rushwa ya waziwazi kwa timu hizo, kwani haiwezekani umfadhili mpinzani wako ambaye unashindana na ukategemea matokeo ya halali.
Yanga ambayo ndio bingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara msimu wa 2015/16 wakiwa wamesalia mechi mbili mkononi itakutana na Ndanda F Jumamosi Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambapo mara baada ya kukamilika kwa mchezo huo, Yanga watakabidhiwa Kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.


No comments:

Post a Comment

advertise here