FACEBOOK Wanasayansi wanadai kuunda aina ya ngozi inayoweza kubandikwa
juu ya mwili wa mtu kupunguza muonekano wa mikunjo ya ngozi mwilini na
ngozi inayopwaya chini ya macho kutokana na uzee.
Ni aina ya
maji maji mtu anayopaka mwilini alafu inaachwa kukauka ambapo baadaye
husihia kuwa ngozi nyembamba iliyo mithili ya 'ngozi ya ujana, Nature
Materials inaarifu baada ya kufanya majiribio kadhaa madogo.
Kwa sasa inafanyiwa majaribio ya kuuzwa kama bidhaa ya urembo.
Lakini wanasayansi Marekani wanasema "ngozi ya pili " huenda baadaye ikaweza kutumika kutengeneza dawa na kinga dhdi ya jua. Ngozi ya pili Kundi
la wanasayansi kutoka chuo kikuu cha Havard kitengo cha matibabu na
taasisi ya teknolojia Massachusetts wamefanya majaribio ya bidhaa hiyo
kwa watu waliojitolea ambao walipakwa ngozi hiyo chini ya macho, kwenye
mikoni yao na miguu.
Ngozi hiyo inayotokana na kemikali
polysiloxane polymer iliundwa kwenye maabara kwa kutumia chembe chembe
za Silicone na hewa safi ya Oxygen.
Licha ya kwamba sio ngozi ya kweli lakini imeundwa kuiga ngozi asili na pia kuacha nafasi ya hewa kupita.
Kwa mujibu wa watatfiti ngozi hiyo bandia ina uwezo wa kunasa mvuke na kusaidia ngozi kujivuta kiasi cha inavyostahili.
Wakati ngozi ikizeeka inanyauka na kwa hivyo haitoi matokeo mazuri vile kwenye majaribio haya.
Watafiti
wanasema ngozi hiyo bandia haionekani na inaweza kubandikwa kwa siku
nzima bila kuwa na madhara yoyote na inaweza kuhimili vitu kama jasho na
mvua.
Lakini utafitia zaidi unahitajika. Ni lazima pia wakaguzi watoe idhini kwamba ni salama kutumiwa.
Dr
Tamara Griffiths wa muungano wa madaktari wa ngozi Uingereza anasema
ngozi ya chini ya macho hupwaya au kufura kutokana na mkusanyiko wa
mafuta katika sehemu hiyo inayohusishwa na uzee.
Licha ya kwamba ni hali ya kawaida lakini watu wengi hujaribu mbinu tofuati kuziondoa, wengine hata kufanyiwa upasuaji.
Dr
Griffiths amesema: "matokeo ya ngozi ya polymer yanayonyesha kuwa
sawana kufanyiwa upasuaji bila ya hatari za upasuaji . Utafiti zaidi
unahitajika, lakini huu ni mtazamo mzuri ulio na matumaini makubwa kwa
tatizo la wengi. Nitafuatilia maendeleo ya utafiti huu kwa makini."
No comments:
Post a Comment