Monday 20 March 2017

MAGUFULI :MAKONDA CHAPA KAZI...HATA MIMI NAANDIKWA KWENYE MITANDAO KWA HIYO NIJIUZULU URAIS????


Rais John Pombe Magufuli amemtaka mkuu wa mkoa wa Dar es salaam kuendelea na kazi na kwamba yeye kama rais hafanyi kazi kwa kuambiwa na mtu kwamba afanye nini



Amesema watanzania wanapoteza muda mwingi kujadili mambo yasiyo ya msingi.


Siwezi nikapangiwa mtu,kwa sababu hata siku ya kwenda kuchukua fomu nilichukua mwenyewe,hakuna mtu aliyenishauri,niliamua mimi mwenyewe kwamba nafiti kuwa 
rais,kwa hiyo nitaamua mwenyewe nani anatakiwa awe wapi,akae wapi?...ni mimi ninayepanga....ninajua wamenielewa kwa hiyo wewe Makonda chapa kazi....nasema chapa kaziii"-Rais Magufuli.

"Suala la kuandikwa kwenye mitandao siyo tija kwangu,hata mimi ninaandikwa kwenye mitandao...kwa hiyo nijiuzulu urais??...Chapa Kazi..hapa kazi tu",-Rais Magufuli.

No comments:

Post a Comment

advertise here