Saturday 27 May 2017

HIVI NANI ANAJUA UNDANI WA ISSUE YA KESI YA BABU SEYA?


Miaka kama saba iliyopita, Mchungaji mmoja Mtu wa makamu, alinisimulia Mkasa wa "Majambazi" waliokuja nyumbani kwake kutaka kumuua maeneo ya Kinondoni. Lakini Kimiujiza "Majambazi" hawa wakashikwa na Usingizi wakakutwa asubuhi na Majirani, "Kumbe hawakuwa Majambazi" bali wale watu wa kazi ambao Wamarekani wanawaita Pigs na Tanzania tunawaita "Mbwa"



Kisa cha Kutaka Kumtoa Roho Baba wa watu, Ilikuwa Binti mmoja Mrembo aliyekuwa na Uhusiano na Ndugu wa Kuzaliwa wa Mheshimiwa saaaana, aliamua kuachana na Maisha hayo. Na kwa sababu ya Vitisho akahamia kwa Familia ya huyu Mchungaji. Sasa mchungaji huyu akawa anapokea Vitisho kuwa ati yeye ndiye aliyemchukulia huyu Bwana mwanamke wake na akaambiwa ataonyeshwa ya Mtema kuni. Baada ya Vitisho kutosaidia ndio hiyo siku ya tukio wakatumwa hao, "Majambazi"

Sasa Nimesikia Kuwa Issue ya Babu Seya na Kina Mramba na Yona, Ni Visasi vya Kiaina hiyo Je Ni kweli?

Pia Nikasikia Kwa wale waliopendwa wakipatikana na matatizo Basi walikuwa wanakufa Kisanii na maiti zao hewa kuzikwa Kisanii under the smoke screen of secrecy!

No comments:

Post a Comment

advertise here